LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 5, 2015

MAGUFULI AACHA GUMZO BABATI MKUTANO WAKE WAHUDHURIWA NA MAELFU YA WAKAZI WA MJI HUO

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa mji wa Babati waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa ameomba nafasi ya Urais ili awatumikie Watanzania katika kuleta maendeleo .
Wakazi wa Babati mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM za kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye uwanja wa Raa,Babati mjini.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa Babati mjini.
 Hivi ndivyo muitikio wa wakazi wa Babati kwenye uwanja wa Raa ulivyokuwa wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Mjumbe wa NEC kutoka Wilaya ya Hanang ,Dk. Mary Nagu akihutubia wakazi wa Babati mjini kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Huu uwanja ni maarufu kwa jina la Raa na hivi ndivyo wakazi walivyojazana kwenye mkutano wa kumnadi mgombea wa urais wa CCM.
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Alhaji Abdalla Bulembo akihutubia wakazi wa Babati mjini kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli ambapo aliwaambaia wananchi hao CCM imemleta mtu anayeendana na wakati kuliongoza Taifa hili.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisali pamoja na Father Dk. Kitima mbele ya kaburi la Mwalimu Abel Amas Hugo ambaye ni mdogo wa Father Kitima .
Mgombea Urais alipita kuwapa pole wakati akiwa njiani kuelekea mkoa wa Manyara akitokea Singida.
 Kaburi la Mwalimu Abel Amas Hugo, aliyezikwa katika kijiji cha Siuyu, Singida Mashariki.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwapa pole ya msiba shangazi wa Father Kitima, Siuyu, Singida Mashariki.



 Wakazi wa Wilaya mpya ya Chemba wakifurahia ujio wa Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Kondoa mjini kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya sabasaba.
 Umati wa wakazi wa Kondoa mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwatambulisha wagombea ubunge wa majimbo ya Kondoa mjini Ndugu Edueni Sannda(kulia) na wa jimbo la Kondoa Vijijini Dk. Ashatu Kamusese (kushoto) kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Sabasaba.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutibia wakazi wa Bereko, Kondoa wakati akiwa njiani kuelekea Babati, mgombea urais wa CCM amefanya zaidi ya mikutano 20 akitokea Singida kuelekea Manyara kupitia Kondoa.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages