LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 28, 2015

MAGUFULI,NAPE ,MWAKALEBELA WAUNGURUMA IRINGA

 Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Iringa mjini kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika uwanja wa Samora.
 Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa ambapo aliwaeleza wananchi wa hapo kuwa ana historia na mkoa huo kwani alisoma hapo na alishafanya mazoezi ya kufundishia hapo hivyo atahakikisha mkoa huo unakuwa vizuri kimaendeleo.
 Sehemu ya Umati wa wakazi wa Iringa mjini waliofurika kumsikiliza Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi mji wa Iringa kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli uliofanyika kwenye uwanja wa Samora.
 Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimtambulisha na mfanyabiashara wa Iringa Salim Abri Asas ambaye ametoa ajira kwa vijana zaidi ya 400 kwenye viwanda vyake .
 Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi ilani ya uchaguzi mgombea ubunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia CCM Frederick Mwakalebela .
 Mgombea ubunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia CCM Frederick Mwakalebela  akiwahutubia wakazi wa mji huo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Samora.

 Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimuombea kura mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini.
 JB akiongea kwa niaba ya Wasanii wenzake wa Filamu za Kibongo wanaowakilisha Team Bajaj ambao wao pia wanamuumnga mkono Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Wasanii wa Fialamu za Kibongo wakipiga push up pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye (mwenye fulana ya kijani.
 Wasanii wakionyesha upendo wao kwa Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli
 Khadija Kopa akishambulia jukwaa pamoja na wanamuziki wengine wa bendi ya TOT.
 Msami akionyesha uwezo wa kuimba na kucheza kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli
 Temba pamoja na Chegge wakishambulia jukwaa pamoja na Ally Yanga (katikati) kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli
 Viongozi wa CCM mkoa wa Iringa wakicheza nyimbo ya CCM mbele kwa mbele


 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Isimani Ndugu William Lukuvi akihutubia wakazi wa Iringa mjini wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli


Mgombea wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akiondoka uwanjani mara baada ya kumaliza kuhutubia.

1 comment:

  1. Mimi nawapongeza kwa jitihada zenu zote za kumpigia campaign mgombea wa chama cha mapinduzi Dr. John Pombe Magufuli tuzidi kumwombea Mungu ashinde kwa kishindo kwenye uchagu ujao CCM oyeeee

    ReplyDelete

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages