LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 30, 2015

MAGUFULI KUUNGURUMA LEO KWENYE UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na mgombea ubunge wa jimbo la Isimani mkoani Iringa Mhe. William Lukuvi kabla ya kuhutubia wakazi wa Kimande kwenye mkutano wa kampeni za CCM zilizofanyika uwanja wa Sabasaba,Kimande isimani mkoani Iringa.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa kata y Migori,Isimani kwenye mkutano wake wa kampeni za CCM.
 Mke wa mgombea ubunge jimbo la Isimani Mhe. Wiliam Lukuvi akimuombea kura kwa wananchi wa Migori kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Migori, Isimani mkoani Iringa.
 Msanii maarufu wa Filamu za kibongo JB ambaye anaongoza timu Bajaji kufanya kampeni za kuinadi CCM akiwasalimu wakazi wa kata ya Migori na kuwataka siku ya tarehe 25 kuipigia kura nyingi CCM.
 Wafanyabiashara ndogo ndogo wa Mtera wakiwa wamemsimamisha Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli ili awasalimie wakati akiwa njiani kuelekea Dodoma mjini.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimsikiliza mgombea ubunge wa jimbo la Kibakwe Ndugu George Simbachawene kabla ya kuhutubia wakazi wa kata ya Chipogolo,wilaya ya Mpwapwa.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM mgombea ubunge wa jimbo la Kibakwe Ndugu George Simbachawene kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika  Chipogolo wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli (katikati) akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Mhe. Adam Kimbisa muda mfupi baada ya kuwasili kwenye uwanja wa mikutano uliopo katika Shule ya Msingi Mvumi Mission.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela kabla ya kuhutubia wakazi wa Mvumi.
 Mgombea ubunge wa jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akihutubia wakazai wa Mvumi kwenye mkutano wa kampeni uliohutubiwa pia na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akihutubia wakazi wa Mvumi kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecelea akisisitiza jambo wakati wa kuhutubia wakazi wa Mvumi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Wakazi wa Mvumi wakishangilia jambo kwenye mkutano wa kampeni za kumnadi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Mvumi ambapo aliwaambia kuwa serikali yake itakuwa ya kuwatumikia Watanzania wote bila kubagua itikadi za vyama vyao ,kabila wala dini.
 Sehemu ya wakazi wa Mvumi waliojitokeza kwenye uwanja wa shule ya Msingi Mvumi Mission kumsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli.
 Wakazi wa Mvumi wakisikiliza sera safi za Chama Cha Mapinduzi kwenye mkutano wa kampeni za CCM ambapo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli aliahidi kuwatumikia Watanzania wote.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde  kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye viwanja vya Mvumi Mission.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. John Pombe Magufuli akiondoka jukwaani mara baada ya kumaliza kuhutubia wakazi wa Mvumi.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages