LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 18, 2015

MAGUFULI APOKELEWA NA MAELFU YA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA

Msafara wa mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli ukiondoka uwanja eneo la uwanja wa ndege wa Mwanza kuelekea ofisi za CCM mkoa wa Mwanza kwa ajili ya kuwasalimu na kujitambulisha kwa wananchi.
Piki piki zikiongoza msafara wa mgombea wa CCM jijini Mwanza.
Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk. John Magufuli akiwapungia mkono wakazi wa Pasiansi waliojitokeza kwa wingi kumlaki.
Mgombea wanafasi ya Urais kwa kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Bwiru waliomsimamisha njiani awasilimia wakati akielekea ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.
Wananchi wa jiji la Mwanza wakishindwa kujizuia na kujikuta wakiusimamisha msafara wa mgombea Urais kupitia CCM,mara kwa mara.




Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Nape Nnuye akishiriki bega kwa bega kuhakikisha mambo yanaenda vizuri.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi aNape Nnauye (kulia)kiwa kwenye gari lililobeba waandishi wa habari




Vijana wa boda boda wa Mwanza mjini katika shamra shamra za kumpokea mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM akiwasili kwenye ofisi za CCM mkoa wa Mwanza tayari kwa kuwasalimu wananchi na kujitambulisha.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Ndugu Rajab Luhavi akiwasalimu wananchi waliojitokeza kwa wingi nje ya jengo la ofisi za CCM mkoa wa Mwanza kumuona mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM DK.John Pombe Magufuli.
Mke wa mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM, Janet Magufuli akiwasalimu wananchi wa Jiji la Mwanza waliojitokeza kwa wingi kuja kumuona mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na wakazi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kwa wingi kumpokea na kumsabahi ambapo aliwashukuru wananchi hao kwa kujitokeza kwa wingi na kuahidi kurudi wakati wa kampeni za Urais zitakapoanza na kuwahakikishia hatowaangusha.




KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages