LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 9, 2015

LUSINDE AWATAKA WATENDAJI KUTEKELEZA MAAGIZO NA AHADI ZA RAIS JIMBONI KWAKE


 Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akielezea maendeleo ya ujenzi wa Shule ya msingi Lowasa kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kijiji cha Muungano wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana(kushoto) akimuonyesha Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde namna ya kufatua matofali wakati wa kushiriki ujenzi wa shule ya msingi Lowasa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupampu maji ya kisima cha mkono kilichopo katika shule ya msingi Mvumi Mission mara baada ya kukagua na kuuzindua mradi huo wa maji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji Bi. Happiness Misile ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule mara baada ya kuzindua kisima cha maji katika shule ya Msingi Mvumi Mission.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi mara baada ya kuzindua kisima cha maji ambapo aliwaambia wananchi hao watunze  sana miundo mbinu ya maji.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Suli kata ya Mvumi Makulu ambapo alijionea ujenzi wa shule ya Msingi Suli unavyoendelea.
 Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mheshimiwa Farida Mgomi akimwagilia maji mti alioupanda katika shule ya Sekondari ya FUFU ikiwa sehemu ya utunzaji mazingira.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpa mkono wa pongezi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Fufu Hassan M.Kilindi kwa kuweza kujenga bweni zuri la wasichana shuleni hapo.
 Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde akicheza ngoma wakati wa kuwasili kwenye uwanja wa mkutano wa hadhara uliofanyika Manzase.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia) akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Chamwino Ndugu Charles Ulanga kabla ya kuhutubia wakazi wa Manzase.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka wilaya ya Chamwino akisalimia wananchi wa Manzase.
 Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusindeakihutubia wakazi wa Manzase ambapo aliwaambia kuwa watendaji wa Serikali wajitahidi kufuata maagizo na maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa wakati.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Manzase na kuwaambia CCM Ipo Imara inajenga nchi na kuwataadharisha vijana wasikimbilie vyama visivyo na sera za maendeleo.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Manzase wilaya ya Chamwino na kwenye mkutano wa hadhara wa CCM ikiwa sehemu ya ziara yake ya kukagua, kusisitiza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010.
 Wazee wakifuatilia kwa makini hotuba ya Kinana.
 Wananchi wa Manzase wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa Manzase ambapo pia aliwasisitiza kujiandikisha kwa ajili ya kupiga kura.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi kadi ya uanachama wa CCM kwa Bi.Roda ambapo zaidi ya wanachama wapaya 750 walijiunga na CCM.
 Katibu Mkuu akiwashukuru wazee wa Manzase mara baada ya mkutano kuisha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mtera Ndugu Livingstone Lusinde wakiwashukuru wananchi mara baada ya kumaliza mkutano katika kijiji cha Manzase,wilaya ya Chamwino.
PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages