LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 7, 2015

KINANA : SIFA KUBWA YA KIONGOZI BORA NI UADILIFU

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiutubia wakazi wa Dodoma mjini kwenye uwanja wa Barafu ikiwa sehemu ya kuimarisha Chama na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010.Kinana aliwaeleza wananchi hao kuwa kiongozi bora ni yule muadilifu.
 Katibu Mkuu wa CCM akihutubia mamia ya wakazi wa Dodoma mjini ikiwa sehemu ya ziara yake mkoani hapo ambapo alisisitiza CCM itasimama imara kuwatetea wanyonge.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Ndugu Adam Kimbisa akiwahutubia wakazi wa Dodoma mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Barafu.
 Balozi Job Lusinde akizungumza na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Dodoma mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Barafu,Nape aliwaambia wakazi hao kuwa makini na wapinzani kwani wamekuwa wakihangahika na fedha za wafadhili ambazo hawaitakii mema nchi yetu.
 Wananchi wakisikiliza hotuba kwa makini.
 Wanachama wapya wakila kiapo kwenye uwanja wa Barafu Dodoma mjini.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wanachama wa CCM Tawi la Bahi Road.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa Chang'ombe ,wilaya ya Dodoma mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa shule ya sekondari Lukundo,Chang'ombe Dodoma mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia bomba la maji linalopita Nzuguni,Dodoma.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia kikundi cha ngoma cha Nuru ambao walikuwa wakiimba wimbo wa Tukupokee kwa Shangwe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amebeba maji tayari kwa kumwagilia nyanya katika shamaba la vijana wajasiriamali wa kijiji cha Nkulabi kata ya Mpunguzi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuchimba mtaro wa maji katika Kata ya Nzuguni, Dodoma mjini.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages