LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 24, 2015

TAMWA YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JUU YA KUPAMBANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA




WENCE AKITOA ELIMU KWA WANAHABARI WALIOKUTANA MKOANI IRINGA
WANAHABARI NWAKIWA MAKINI KUMSIKILIZA MTOA ELIMU
MWANAHABARI FRANK KIBIKI AKIWA MAKINI KUFUATILIA NINI KINACHOENDELEA KWENYE MAFUNZO HAYO

 NA fredy mgunda,iringa

Waandishi wa habari wametakiwa kuandika zaidi habari zinazohusu unyanyasaji wa kijinsia hususan dhidi ya wanawake na watoto ili kuiamsha zaidi jamii inayowafanyiwa vitendo hivyo na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya vitendo hivyo.

Msisitizo huo ulitolewa na chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) kwa waandishi wa habari wa mikoa ya nyanda za juu kusini (IRINGA,MBEYA,SONGEA NA NJOMBE) ambapo wanahabari wameombwa kuendelea kufichua habari hizo hususan kwa wanaofanyiwa vitendo hivyo ili waweze kuelewa kwamba sheria dhidi ya ukatili huo zipo na kwamba kuna taasisi za kuwatetea.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo mwanahabari wa siku nyingi WENCE MUSHI alisema dhahiri kuwa vitendo vya unanyanyasaji vimepungua kutokana na wanaofanya ukatili huo kuelewa, na watendewa pia kuzidi kuamka, juhudi zaidi zilitakiwa kujipenyeza zaidi dhidi ya imani za kimila ambazo bado zinashikiliwa katika sehemu mbalimbali za nchi.

“Endeleeni kutumia kalamu zenu na vifaa vyenu vyote kupiga vita vitendo vyote vinavyotokana na manyanyaso ya kijinsia ambayo hasa hutokana na mfumo dume,” alisema wence akiwaomba wahabari kufanya hivyo kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kutokomeza kabisa suala la unyanyasaji wa kijinsia.

Wence alisema jicho la waandishi wa habari linasaidia kuwaelimisha wananchi juu ya mambo mbalimbali yanafanywa kinyume cha seria,kuwaomba wanahabari kufanya habari za kichunguzi juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na unyanyasaji wake.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa TAMWA imekijita katika kufuatilia habari juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na mauwaji ya watu wenye ulemavu na kulenga hasa habari za kichunguzi ambazo zitaleta mabadiliko kwa jamii yetu.

Kwa upande wa waandishi wa habari wa nyanda za juu kusini walioshiriki warsha hiyo wamesema kuwa wanafanya kazi hiyo katika mazingira magumu,hivyo kuwaomba TAMWA kuwasaidia chombo cha usafiri kila mkoa ili waweze kuwafikia wananchi waliopo vijijini na kupata taarifa zao.

Lakini wakawataka wanahabri wengine kufanya kazi kwa kufuta weledi wao kutokana na elimu walioipata wakiwa darasa na kwenye mafunzo mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages