LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 4, 2015

SERIKALI YAWAREJESHEA KIWANDA CHA CHAI WANANCHI WA MPONDE


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akiwasili mkoani Tanga ambapo alipokelewa Segera kijiji cha Mchungwani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Tanga Aisha Kigoda mara baada ya kuwasili mkoani Tanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Tanga Mjini Omary Nundu wakati wa mapokezi yaliofanyika Segera kijiji cha Mchungwani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Mchungwani kata ya Segera waliojitokeza kumpokea akiwa njiani kuelekea Mponde jimbo la Bumbuli.
 Gari iliyombeba Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye uwanja wa mkutano kijiji cha Mponde jimbo la Bumbuli.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa Wakulima Halmashauri ya Bumbuli Almasi Kassim wakati akiwasili kwenye uwanja wa mikutano wa kijiji cha Mponde.
 Sehemu ya Umati wa wakazi wa kijiji cha Mponde waliojitokeza kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu  Abdulrahman Kinana ambaye amerudi Mponde kutimiza ahadi yake ya kurudi na kulizungumzia suluhisho la mgogoro wa kiwanda cha Chai cha Mponde.
 Wananchi wakinyoosha mikono juu kama ishara ya kumsalimia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mhe. Majid Hemed Mwanga akisalimia wananchi wa Mponde waliojitokeza kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyerejea kijijini hapo kutimiza ahadi yake ya kurejea .

 Msanii aliyevaa kinyago usoni akiigiza kama muwekezaji wa chai Mponde.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Mponde ambapo aliwaambia Serikali imerudisha kiwanda cha chai cha Mponde kwa wananchi hao.
 Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Chai Tanzania Mathias Assenga Benedict akisalimia wananchi wa Mponde mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,
 Mkurugenzi Mkuu wa Maendeleo ya wakulima wadogo wa chai Tanzania Ndugu Mustafa  Umande akisalimia wananchi wa Mponde.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Mponde.
 Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh.January Makamba akiwasalimia wananchi wa Mponde ambapo alimshukuru Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa kazi nzuri ya kujenga na kuimarisha chama.
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Mponde na kuwataka kuwa na umoja na ushirikiano na kuepuka watu watakaotaka kutumia fursa hiyo ya umiliki wa kiwanda .

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages