LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 18, 2015

KINANA AWATAKA VIONGOZI KUWA WAADILIFU DIMANI ZANZIBAR

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanachama na wapenzi wa CCM mara baada ya kuwasili kwenye mkoa wa Magharibi tayari kwa ziara ya kujenga na kuimarisha chama mkoani humo.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Magharibi Yusuph Mhamed Yusuph akisalimia wajumbe wa kikao cha halmashauri kuu ya wilaya na kumkaribisha  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuongea na wajumbe hao
 Mlezi wa CCM mkoa wa Magharibi ambaye pia ni Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya ya Dimani jimbo la Kiembesamaki.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya ya Dimani na kuwaambia kuwa kila kiongozi wa CCM anapaswa kuwa mwadilifu kwani Watanzania wanapenda uadilifu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Idd mara baada ya kumaliza kikao cha halmashauri kuu ya wilaya ya Dimani
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd mara baada ya kumaliza kikao cha halmashauri kuu ya wilaya ya Dimani,mkoa wa Magharibi,Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Meneja Uzalishaji  Ndugu Kirtikumar B.Dave juu ya  maziwa yanayotengenezwa katika Kiwanda kipya cha Azam Dairy Products Limited kilichopo  Fumba, Unguja Zanzibar.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongea na Viongozi,Walimu na wanafunzi wa chuo cha Sayansi ya Bahari kilichopo Shakani ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani Magharibi ,Zanzibar.
 Walimu,watumishi na washika dau wengine wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM alipokuwa anazungumza nao katika Chuo cha Sayansi ya Bahari kilichopo Shakani, Zanzibar.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akishiriki usafi wa mazingira kwa kufyeka majani katika mazingira yanayozunguka chuo cha sayansi ya bahari kulia ni Profesa David Mfinanga Naibu Makamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mikoko Fuoni Kibondeni ,Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Magharibi Ndugu Yusuph Mohamed Yusuph.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuweka kaa kama ishara ya kutunza viumbe hao.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuweka kaa kama ishara ya kutunza viumbe hao katika eneo la Fuoni Kibondeni.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipita kwenye mikoko kuangalia jitihada za kutunza mazingira zinavyofanyika  Fuoni Kibondeni
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akinywa dafu mara baada ya kumaliza shughuli za kutunza mazingira mabapo alipanda mikoko pamoja na kuweka kaa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akila dafu mara baada ya kumaliza zoezila utunzaji mazingira na kupanda mikoko Fuoni Kibondeni.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akila kwa mara ya kwanza chakula kilichopikwa kutokana na kiumbe wa baharini ajulikanaye kama Suka.
 Pichani ,Suka akionyeshwa kwa Katibu Mkuu, Suka ni chakula maarufu sana kwa wakazi wa pwani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanan akizungumza na wananchi wa Fuoni Kibondeni ambapo aliwasisitiza waendelee kutunza mazingira kwani mazingira ni muhimu kwa maisha ya kila siku ya wanaadamu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wana CCM wa Tawi la Kijito Upele jimbo la Fuoni.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wana CCM wa tawi la Tungujani.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ofisi ya CCM tawi la Tungujan.
 Wana CCM wa Jimbo la Kiembesamaki wakionyesha ujumbe wa kuunga mkono Katiba iliyopendekezwa.
 Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Zanzibar) Shaka Hamdu Shaka akihutubia wakazi wa Jimbo la Dimani kwenye uwanja wa Magereza Tomondo.
 Wananchi wakionyesha alama ya serikali mbili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Magereza Tomondo
 Wananchi wakifuatilia kwa makini.
 Wazee nao walikuwa makini na hotuba za viongozi wao.
 Balozi Ali Karume akihutubia wakazi wa jimbo la Dimani ambapo aliwaambia Katiba iliyopendekezwa ni Katiba bora na kuwataka Wazanzibar kuisoma na kuielewa vizuri.


 Shamsi Vuai Nahodha akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa Magereza Tomondo kuja kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

 Katibu wa NEC Itikadi Na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa wilaya ya Dimani mkoa wa Magharibi ambapo aliwaeleza hesabu na sayansi ya kisiasa imewamaliza wapinzani hivyo CCM itashinda uchaguzi ujao.
 Huu ni mzuka wa mwana CCM kwenye mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana uliofanyika Tomondo, Dimani, Zanzibar.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Zanzibar, Dkt. Mwinyi Haji Makame akihutubia kwenye mkutano huo ambapo alisema muda umefika wa kurudisha majimbo yote Zanzibar yaliyochukuliwa na wapinzani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye viwanja vya magereza Tomondo ambapo aliwaambia CCM ya sasa inazingatia uadilifu na maadili.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Dimani mkoa wa Magharibi Zanzibara na kuataka wana CCM kushikamana huku akiwaambia vijana kuwa wasiwewanyonge katika kukitetea chama chao.
 Mamia ya watu wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM kwenye viwanja vya Magereza ,Tomondo wilaya ya Dimani mkoa wa Magharibi Zanzibar.
Wanachama wapya zaidi ya 600 wa CCM na jumuiya zake wakila kiapo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages