LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 14, 2015

KINANA AANZA ZIARA ZANZIBAR

  • Apata mapokezi wakubwa wilaya ya mjini
  • Ashiriki kazi za kijamii
  • Asisitiza viongozi wasaidie wananchi kuipata,kuisoma na kuielewa Katiba iliyopendekezwa kwani ina masuala yote ambayo Wazanzibari wanahitaji
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu na kijana wa Chipukizi kama ishara ya kukaribishwa Wilaya ya Mjini katika Tawi la mjini ambapo alisomewa taarifa fupi za chama na serikali juu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.
 Mwanachama wa CCM akiwa amejipamba kwa aina yake wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa katika tawi la Kilimani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima kwa kupiga saluti wakati wa mapokezi katika tawi la Kilimani wilaya ya Mjini Zanzibar.


 Katibu Mkuu wa CCM akiangalia ngoma ya Msewe wakati wa mapokezi katika jimbo la Jang'ombe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu akiwapungia mkono wananchi wa jimbo la Jang'ombe walijitokeza kumpokea kwenye jimbo lao,wilaya ya Mjini Zanzibar.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi jezi na mipira kwa timu ya Jang’ombe 503 kwa kiongozi wa timu hiyo Edward Mwingira
 Mbunge wa Jimbo la Kwahani ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi akisalimia wananchi wakati wa uzinduzi wa kuzindua mradi wa maji.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimia wananchi wa jimbo la Kwahani wilaya ya Mjini Zanzibar wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji na uchimbaji mifereji sambamba na kutandaza mabomba.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Matarumbeta jimbo la Kwahani kabla ya kuzindua mradi wa maji na kushiriki uchimbaji mitaro na kusambaza mabomba.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages