LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 28, 2014

KINANA ATAKA BAADHI YA SHERIA ZINAZOHUSU WAKULIMA WA KOROSHO ZIANGALIWE UPYA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumpokea wakati akiwasili wilaya ya Mtwara kijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Mtwara vijijini ,Katibu Mkuu wa CCM anazunguka nchi nzima kufuatilia utekelezaji wa ilani na kuimarisha chama chetu.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye akisisitiza wananchi wa kata ya Nanyamba kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wakazi wa kata ya Nanyamba ,Mtwara vijijini ikiwa sehemu ya ziara yake ya kujenga na kuimarisha Chama.
Ujenzi wa  Wodi za wagonjwa kituo cha afya kata ya Nanguruwe wilaya ya Mtwara vijijini ukiwa unaendelea kwa kasi nzuri.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa wodi ya wagonjwa ya kituo cha afya cha Nanguruwe kutoka kwa Mganga Mfawidhi Dk.Issa Lipupu,Katibu Mkuu wa CCM anaendelea kukijenga chama kwa kukagua ilani ya uchaguzi ya CCM 2010.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye akiwasalimia wakazi wa kata ya Nanguruwe wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa CCM kwenye wilaya ya Mtwara Vijijini,tarehe 28 Novemba 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wakazi wa kata ya Nanguruwe ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa kuna sheria zinazomkandamiza mkulima inabidi zitazamwe upya kwani zisipobadilishwa mkulima atakuwa anakandamizwa kila siku na kutoona faida ya kuwa mkulima wa korosho.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mnara wa shujaa Ahamad Mzee aliyepambana na Wareno waliokuwa wanataka kuivamia Tanzania mwaka 1972 mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.


  Wananchi wa kijiji cha Kitaya mkoani Mtwara wakishangilia ujio wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye kijiji hicho kinachopakana na nchi ya Msumbiji.
 Wasanii wa kikundi cha ngoma cha Kitaya wakitumbuiza kwenye uwanja wa mikutano ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyefika kijijini hapo kujionea uhai wa chama na kuangalia maendeleo ya utekelezaji wa ilani.
 Wageni kutoka nchi jirani ya Msumbiji wakisimama wakati wa utambulisho.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Kitaya wilaya ya Mtwara Vijijini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Kitaya kilichopo mpakani na nchi ya Msumbiji ikiwa sehemu ya ziara yake mkoani Mtwara ambapo anakagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi pamoja na kujenga na kuimarisha chama.
 Wananchi wa kijiji cha Kitaya wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa anawahutubia wakazi wao ikiwa sehemu ya ziara yake ya kujenga na kuimarisha chama.
 Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Wilman Ndile akihutubia wananchi wa Kitaya ambapo aliwaambia mipango ya maendeleo na utekelezaji wake unaendelea vizuri kwenye miradi yote ambayo iliahidiwa na serikali.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wa kijiji cha Kitaya wilaya ya Mtwara Vijijini.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na Makatibu Kata waliokabidhiwa pikipiki kwa ajili ya kufanikisha utendaji wao, ambapo pikipiki 28 zilikabidhiwa.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages