HABARI MPYA

Your Ad Spot

Jul 10, 2014

KINANA AFANYA MAZUNGUMZO NA MGOMBEA WA URAIS WA MSUMBIJI KWA TIKETI YA FRELIMO JIJINI DAR ES SALAAM


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mgombea wa Urais wa Msumbiji Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi kwenye hotel ya Golden Tulip ambapo alikuwa na mazungumzo naye .
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria akisalimiana na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya Frelimo Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi, kabla ya kuanza mazungumzo kwenye hoteli ya Golden Tulip.
 Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya Frelimo Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari ambao walitaka kufahamu mahusiano yao na CCM pamoja na namna Demokrasia inavyoendeshwa nchini Msumbiji,Mheshimiwa Nyusi alisema mahusiano yao na CCM ni mazuri na ya kihistoria Tangia wakati wa mapambano ya Ukombozi,alipoulizwa kuhusu uwezo wake wa kuongea Kiswahili vizuri alisema wakati wa mapambano ya Ukombozi aliwahi ishi Tunduru na Nachingwea nchini Tanzania.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dr.Asha-Rose Migiro(Kulia),Katibu wa NEC Oganizesheni Dr.Mohamed Seif Khatibu na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Maofisa wengine wa Chama Cha Mapinduzi kwenye meza ya mazungumzo na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya chama cha Frelimo Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi na Ujumbe wake kwenye ukumbi wa  Nyerere,Golden Tulip Hotel.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dr.Asha-Rose Migiro(Kulia),Katibu wa NEC Oganizesheni Dr.Mohamed Seif Khatibu na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye meza ya mazungumzo na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kwa tiketi ya chama cha Frelimo Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi na Ujumbe wake kwenye ukumbi wa  Nyerere,Golden Tulip Hotel.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages