LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 20, 2013

KINANA AAHIDI UTUMISHI ULIOTUKUKA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Ndugu Jestina Mhagama mara baada ya kuwasili katika eneo la Seminari Kuu wilaya ya Peramiho.
 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akisalimiana na Mbunge wa Peramiho Ndugu Jenista Mhagama .
 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye mavazi ya jadi yajulikanayo kama Mgolole na kukabidhiwa silaha za jadi alipowasili katika kijiji cha Peramiho B.

 Wanachama wa shina namba 28 wakishangilia hotuba ya  Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye yupo kwenye ziara ya kukagua uhai wa chama katika Mkoa wa Ruvuma.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akinywa chai nyumbani kwa Balozi wa Nyumba 10 Issa Said,Katibu Mkuu amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mabalozi wa nyumba 10 wanatembelewa na viongozi wa ngazi zote.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na viongozi na wananchi wa Peramiho wakishiriki kubeba matofali ya ujenzi wa Zahanati ya Kahegwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kata ya Kahegwa baada ya kushiriki shughuli za kubeba matofali kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Kahegwa,Katibu Mkuu aliwaeleza wananchi hao kuimarisha moyo wa kujitegemea  kwani maendeleo ya Tanzania yataletwa na Watanzania wenyewe na si wahisani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akizungumza na mmoja wa wananchi aliyefarijika sana kwa kumsikia Katibu Mkuu akizungumza maneno ya msingi na yenye kutia moyo sana hasa katika suala la kujitegemea.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti kwenye zahanati ya Lusonga ambayo kwa asilimia kubwa imejengwa kwa nguvu za wananchi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Ndugu Jenista Muhagama ,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma Ndugu Oddo Mwisho na wakikata utepe wa kufungua jengo la Zahanati ya   Lusonga.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisiliza taarifa ya kikundi cha akina mama wajasiriamali  watengeneza sabuni ambayo ilisomwa na Fransisca Andrea.
 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi la jengo la  Ofisi ya tawi la Mlandizi, Peramiho wilaya ya  Songea vijijini.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Peramiho ,wilaya ya Songea Vijijini  mkoani Ruvuma.
 Mbunge wa Jimbo la Peramiho  Ndugu Jestina Muhagama akihtubia wakazi wa Peramiho na kuzungumzia matatizo sugu yanayo wasunbua wananchi wa jimbo lake hasa ukosekanaji wa Pembejeo na kutolipwa pesa wanayodai serikali kwa wakati.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Peramiho ambapo aliwapongea kwa kuwa wakulima wazuri


 Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk.Asha-Rose Migiro akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Tarafa Ndugu Salima Mapunda baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara.



 Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya kufungua jengo la CCM Tawi la Masangu.
 Katibu Mkuu wa CCm Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na masista  kutoka kanisa katoliki la Chikole,jimbo la Peramiho.


No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages