LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 29, 2020

WAPIGA KURA KUHAKIKI BURE TAARIFA ZAO KWA KUTUMIA SIMU,TOVUTI

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu, Semistocles Kaijage akizungumza wakati wa mkutano na Viongozi wa Vyama vya Siasa kuhusu mafanikio ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Nec, Dk.  Wilson Charles Mahera.



Na Richard Mwaikenda

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeanisha njia tatu za Mpiga Kura kumwezesha kuhakiki kirahisi taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Awamu ya Pili katika zoezi linalotarajiwa kuanza Aprili 17 mwaka huu.

Njia hizo ni; kuhakiki taarifa zao katika orodha itakayokuwa imebandikwa katika vituo,kutumia mfumo wa Voters’ Interaction Systems  (VIS), ambapo Mpiga kura kupitia simu yake ya kiganjani atapiga namba *152*00# na  kufuata maelekezo. Huduma hii ni ya bure. Vilevile, kwa kupitia Tovuti ya Tume (_HYPERLINK "http://www.nec.go.tz"_www.nec.go.tz_),atahakiki taarifa zake katika sehemu iliyoandikwa “uhakiki” na kuendelea kufuata maelekezo.


Pia, Wapiga Kura  watahakiki kupitia kituo cha Huduma kwa Wapiga Kura (Call centre) ambapo wananchi watapiga simu bure kupitia namba ya simu ya kituo ambayo ni 0800782100 na kupata usaidizi katika kuhakiki taarifa zao.

Njia hizo zilitajwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu,Semistocles  Kaijage wakati wa mkutano na Viongozi wa Vyama vya Siasa wa kuwapa taarifa kuhusu mafanikio ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Kaijage alisema kuwa,Tume imeweka njia zote hizo ili iwe rahisi kwa Wapiga Kura wote kuhakiki taarifa zao.

Alisema kuwa,Daftari la Awali litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha Wapiga Kura katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza, lakini uboreshaji wa Daftari wa Awamu ya Pili na uwekaji wa Pingamizi utafanyika katika vituo vilivyoteuliwa na Tume katika kila Kata.

Idadi ya Vituo hivyo nchi nzima  ni Elfu nane na thelathini na moja (8031).


"Katika vituo hivyo kutakuwa na BVR Kits kwa ajili ya kufanya marekebisho husika.  Kwa hiyo, Mpiga Kura aliyehakiki taarifa zake kwa kutumia njia yoyote kati ya hizo tatu zilizotajwa na  kuhitaji kurekebisha taarifa zake, basi atakwenda kwenye kituo kilichoteuliwa kwa ajili ya zoezi hilo,"alisema Kaijage.


Kwa mara nyingine ,Mwenyekiti huyo wa Tume aliwaeleza viongozi hao wa vyama jinsi Tume kuhusu ukamilishwaji wa maandalizi kwa ajili ya zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili.

Alisema kwa mujibu wa Kifungu cha 15 (5) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na Kifungu cha 21(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Tume inapaswa kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara  mbili kati ya Uchaguzi Mkuu mmoja na unaofuatia.

 Aliwataja watakaohusika katika uboreshaji wa awamu hii,kuwa ni; Wapiga Kura wapya ambao  ni raia wa Tanzania waliotimiza umri wa miaka 18 au watatimiza umri huo siku ya Uchaguzi Mkuu,waliohama kutoka maeneo yao ya awali na kuhamia maeneo mengine ya kiuchaguzi, na wale ambao  kadi zao zimeharibika au kupotea. 

 Zoezi pia litahusisha kuwaondoa kwenye Daftari, Wapiga Kura waliofariki na wengine waliopoteza sifa kwa mujibu wa sheria.

Vile vile, awamu hii itawahusu Wapiga Kura ambao hawakupata fursa kujiandikisha katika Awamu ya Kwanza, yaani Wapiga Kura wapya au wale waliotaka kurekebisha taarifa zao.


Uboreshaji wa Daftari  Awamu ya Pili ambao utaenda sambamba na Uwekaji wazi wa Daftari la Awali utafanyika  katika “routes” tatu. Route  ya kwanza inatarajiwa kuanza tarehe  17 Aprili, 2020.

Katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya pili, vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa  saa 12:00 jioni kwa muda wa siku nne (4) mfululizo. 



WAPIGA KURA KUHAKIKI BURE TAARIFA ZAO KWA KUTUMIA SIMU,TOVUTI

Na Richard Mwaikenda

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeanisha njia tatu za Mpiga Kura kumwezesha kuhakiki kirahisi taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Awamu ya Pili katika zoezi linalotarajiwa kuanza Aprili 17 mwaka huu.

Njia hizo ni; kuhakiki taarifa zao katika orodha itakayokuwa imebandikwa katika vituo,kutumia mfumo wa Voters’ Interaction Systems  (VIS), ambapo Mpiga kura kupitia simu yake ya kiganjani atapiga namba *152*00# na  kufuata maelekezo. Huduma hii ni ya bure. Vilevile, kwa kupitia Tovuti ya Tume (_HYPERLINK "http://www.nec.go.tz"_www.nec.go.tz_),atahakiki taarifa zake katika sehemu iliyoandikwa “uhakiki” na kuendelea kufuata maelekezo.


Pia, Wapiga Kura  watahakiki kupitia kituo cha Huduma kwa Wapiga Kura (Call centre) ambapo wananchi watapiga simu bure kupitia namba ya simu ya kituo ambayo ni 0800782100 na kupata usaidizi katika kuhakiki taarifa zao.

Njia hizo zilitajwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu,Semistocles  Kaijage wakati wa mkutano na Viongozi wa Vyama vya Siasa wa kuwapa taarifa kuhusu mafanikio ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Kaijage alisema kuwa,Tume imeweka njia zote hizo ili iwe rahisi kwa Wapiga Kura wote kuhakiki taarifa zao.

Alisema kuwa,Daftari la Awali litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha Wapiga Kura katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Kwanza, lakini uboreshaji wa Daftari wa Awamu ya Pili na uwekaji wa Pingamizi utafanyika katika vituo vilivyoteuliwa na Tume katika kila Kata.

Idadi ya Vituo hivyo nchi nzima  ni Elfu nane na thelathini na moja (8031).


"Katika vituo hivyo kutakuwa na BVR Kits kwa ajili ya kufanya marekebisho husika.  Kwa hiyo, Mpiga Kura aliyehakiki taarifa zake kwa kutumia njia yoyote kati ya hizo tatu zilizotajwa na  kuhitaji kurekebisha taarifa zake, basi atakwenda kwenye kituo kilichoteuliwa kwa ajili ya zoezi hilo,"alisema Kaijage.


Kwa mara nyingine ,Mwenyekiti huyo wa Tume aliwaeleza viongozi hao wa vyama jinsi Tume kuhusu ukamilishwaji wa maandalizi kwa ajili ya zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili.

Alisema kwa mujibu wa Kifungu cha 15 (5) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na Kifungu cha 21(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Tume inapaswa kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara  mbili kati ya Uchaguzi Mkuu mmoja na unaofuatia.

 Aliwataja watakaohusika katika uboreshaji wa awamu hii,kuwa ni; Wapiga Kura wapya ambao  ni raia wa Tanzania waliotimiza umri wa miaka 18 au watatimiza umri huo siku ya Uchaguzi Mkuu,waliohama kutoka maeneo yao ya awali na kuhamia maeneo mengine ya kiuchaguzi, na wale ambao  kadi zao zimeharibika au kupotea. 

 Zoezi pia litahusisha kuwaondoa kwenye Daftari, Wapiga Kura waliofariki na wengine waliopoteza sifa kwa mujibu wa sheria.

Vile vile, awamu hii itawahusu Wapiga Kura ambao hawakupata fursa kujiandikisha katika Awamu ya Kwanza, yaani Wapiga Kura wapya au wale waliotaka kurekebisha taarifa zao.


Uboreshaji wa Daftari  Awamu ya Pili ambao utaenda sambamba na Uwekaji wazi wa Daftari la Awali utafanyika  katika “routes” tatu. Route  ya kwanza inatarajiwa kuanza tarehe  17 Aprili, 2020.

Katika Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya pili, vituo vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi na kufungwa  saa 12:00 jioni kwa muda wa siku nne (4) mfululizo. 



 

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages