LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 9, 2018

TANESCO YAIBUKA KIDEDEA MAONESHO YA NANE NANE SIMIYU


Meneja wa TANESCO Mkoa wa Simiyu Bi. Rehema Mashinje (mwenye fulana ya mistari), akiungana na wafanyakazi wa Shirika hilo kusherehekea ushindi wa kwanza (kipengele cha mashirika ya serikali), kwakuwa banda bora kwenye maonesho ya Wakulima Nanenane mwaka 2018 yaliyoadhimishwa kitaifa Mkoani Simiyu Agosti 8, 2018.
NA SAMIA CHANDE, SIMIYU
SHIRIKA LA UMEME NCHINI, (TANESCO),  limeibuka mshindi wa kwanza katika kipengele cha Mashirika ya Serikali kwenye maonesho ya wakulima ( NANE  NANE) katika viwanja  vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu ambapo kauli mbiu ya mwaka 2018 ni “Wekeza katika kilimo mifugo na uvuvi  kwa maendeleo ya viwanda”.
Katiaka maonesho hayo TANESCO iliweza kutoa elimu mbalimbali kuhusu umeme pamoja na matumizi bora ya umeme.
Meneja wa TANESCO mkoani Simiyu Bi. Rehema Mashinje alisema katikanmaonyesho haya Nane Nane TANESCO tumejipanga kutoa  huduma bora na kwa welendi mkubwa.
Pia alitoa rai kwa kwa mananchi wote kutumia fulisa hii ya nane nane kutembelea banda la TANESCO ili kupata elimu mbalimbali kuhusu maswala ya umeme hususani  kuhusu miradi ya umeme  vijiji(REA) ili kuhakikisha kila wananchi wote wanaopitiwa na mradi wa Umeme Vijini( REA) wanaonganishwa na huduma hiyo mara moja.
Aliongezea kwa kusema  bila umeme hamna kitu kinaweza kuendelea hivyo wananchi walime kwa bidi ilitupate mazao mengi  tuweze kuendeleza viwanda vyetu na sisi TANESCO tumejipanga kuhakikisha viwanda vyote vinapata umeme wa uhakika.
TANESCO kama mdau muhimu iliweza kuhakikisha mabanda yote katika viwanja vya Nyakabidi vinapata umeme wa uhakika muda wote.
Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba  alifungua rasmi maonyesho katika hotuba yake alitoa wito kwa wananchi wote wa mikoa inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga Kutumia  fursa  ya kutembelea katika maonyesho hayo ili kujifunza mbinu mbalimbali za kitaalamu katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.
Katika kufunga maonyesho raisi Mtahafu wa awamu ya tatu Mhe. Benjamini William Mkapa alisema kua kiwanja  hiki cha Nyakabindi kitumike kama darasa la wakulima, wavuvi na wafugaji.
 Meneja wa TANESCO Mkoa wa Simiyu Bi. Rehema Mashinje pamoja na Mkurugenzi wa REA Bwana Amos Manga  wakisherekea Ushindi katika maonyesho ya Nane Nane katika viwanja vya Nyakabindi

 Wananchi wakiwa wamefurika kwenye banda la TANESCO ili kupatiwa habari mbalimbali zihusuzo huduma zitolewazo na Shirika hilo.
 Wananchi wakiwa wamefurika kwenye banda la TANESCO ili kupatiwa habari mbalimbali zihusuzo huduma zitolewazo na Shirika hilo.

 Wanafunzi wa Simiyu Golden Open School wakiwa wamekabidhiwa madafutari katika banda la TANESCO bada ya kujibu kwa usahihi maswali kuhusu umeme na matumizi yake.(PICHA NA SAMIA CHANDE)




No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages