LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 2, 2018

JAKAYA MRISHO KIKWETE FOUNDATIONI YASAINI MKATABA WA MOU NA BALOZI WA KUWAIT

Rais Msaafu Jakaya Kikwete akishuhudia uwekaji saini kati ya Balozi wa Kuwait, Jasem Al-Najem (wa kwanza kushoto)  na Mkurugenzi wa Taasisi ya Jakaya Kikwete Foundation, Omari  Issa wapili kulia  kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo na wenye ulemavu wa ngozi (ALBINO) wenye thamani ya Milioni 90. wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suleiman Sale
Rais Msaafu Jakaya Kikwete akishuhutia Balozi wa Kuwait, Jasem Al-Najem (wa kwanza kushoto)  na Mkurugenzi wa Taasisi ya Jakaya Kikwete Foundation, Omari  Issa wa pili kulia wakionyesha mikataba hiyo kwa wanahabari (pichani hawapo) mara baada ya kusaini mkataba kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo na wenye ulemavu wa ngozi (ALBINO) wenye thamani ya Milioni 90. wa kwanza kulia ni, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suleiman Sale 

Rais Msaafu Jakaya Kikwete akishuhutia Balozi wa Kuwait, Jasem Al-Najem (wa kwanza kushoto)  na Mkurugenzi wa Taasisi ya Jakaya Kikwete Foundation, Omari  Issa wa pili kulia wakikabidhiana mkataba huo mara baada ya kusaini mkataba kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo na wenye ulemavu wa ngozi (ALBINO) wenye thamani ya Milioni 90. wa kwanza kulia ni, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Suleiman Sale 
Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete katikapicha ya pamoja na viongozi hao


Kwanza namshukuru Balozi wa Kuwait wamekuwa wakitoa misaada mingi kwa maendeleo ya Jamii na kuendelea kutowa misaada mikibwa kwa Serikali kwa kujenga Barabara, Madaraja kwa kipindi nilipokuwa, Rais Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri wa Fedha tumenufaika sana, sasa wamekuja na misaada ya kusaidia Jamii na huu tunaoupokea leo ni kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa viungo wenzetu wenye ulemavu wa ngozi, Na wamependa kusaidi katika Foundation yetu ya  Jakaya Kikwete na tutafikisha kwa wanao husika, Na ninawashukuru kwa Moyo wao wa upendo kwa kuguswa na ndugu zetu wenye ulemavu na kuna wanahitaji msaada na wamejitolea na kuomba kukutana nami na nikamwambia nje na sasa nimezungumza na Balozi nataka tufanye mambo makubwa ya kufanya kati ya Foundation yetu na Ubalozi wa Kuwait na mashirika mbalimbali yasiyo ya Kiserikali ya Kuwait yanayoshughulika na maswala ya akinamama na watoto, Afya ya akina Mama na watoto, yanayoshughulika na kuendeleza vijana iliwaze kupata maendeleo na kujiajiri na yanayoshughulika na wakulima wadogo wadogo kushughulika na maswala mengineyo naamini kwa shughuli tunazozifanya   kwa kupata ushirikiano na michango kwa Balozi tunaweza kufanya mambo makubwa zaidi, lakini leo nato shukrani nyingi sana kwa Ubalozi wa Kuwait na Serikali ya Kuwait kwa msaada huu, Inaweza kuoneaka mdogo lakini inawafanya waweze kuishi maisha yenye nafuu zaidi na asanteni sana

Kwa napenda kutoa Shukrani za dhati kabisa tukiwa na Mhe, Rais Mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kutia saini mkataba wa MOU kati ya Ubalozi wa Kuwait na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation ikiwa lengo na madhumuni nikuweza kusaidia nduguzetu, vijana wetu, watoto wetu wenye ulemavu wa viungo na wenye ulemavu wa ngozi (ALBINO), ambapo mkataba huu ni wenye thamani ya Milioni 90 lengo ni kusaidia vijana wetu ambao wanaulemavu wa aina mbalimbali, Hakika hatua hii ya leo ni mwanzo wa ushirikiano kati ya Serikali ya Kuwait kupitia ubalozi wake uliopo hapa Dar es Salaa na Taasisi ya Jakaya Kikwete Foundation na nimwanzo tunaotarajia utakuwa mwema na utakaozaa matunda na kwa kupitia hatua hii bilashaka ushirikiano huu utaendelea kati ya Ubalozi wa Kuwait na Taasisi hii  pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali ya Kuwait kuweza kushirikiana kwa maoja na Taasisi hii, misaada hiyo ni ibara ya vifaa , zana na nyenzo ambazo zitawasaidia nduguzetu, watoto wetu vijana walemavu Albino, kwa hiyo ni ibara ya vifaa na zana kwa ajili ya kundihilo lenye mahitaji maalumu




Mhe, Rais Mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na viongozi hao. PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA 

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages