LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 30, 2018

TAGCO NA IDARA YA HABARI MAELEZO CHACHU YA MAGEUZI UTENDAJI WA MAAFISA HABARI

 Mkurugenzi wa Halmashuri ya Manispaa ya Songea Bi.Tina Sekambo akisisitiza kuhusu namna Manispaa hiyo inavyomuwezesha Afisa Habari wake kutekeleza jukumu la kuisemea Serikali kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa manufaa ya wananchi.
 Muwakilishi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Casmir Ndambalilo akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi wa Halmashuri ya Manispaa ya Songea Bi.Tina Sekambo  wakati wa ziara ya ujumbe kutoka chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO)

 Mkurugenzi wa Halmashuri ya Manispaa ya Songea Bi.Tina Sekambo (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) mara baada ya ziara ya ujumbe huo katika manispaa hiyo, ziara hiyo imelenga kukagua na kuona utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano katika manispaa hiyo na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla ili kuweka mikakati ya pamoja ya kuimarisha mfumo wa utoaji wa taarifa za miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika Halmashuri hiyo.

Kiongozi wa ujumbe wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza umuhimu wa Halmashuri kuwaruhusu maafisa Habari kushiriki katika Kikao Kazi cha mwaka ili wajengewe uwezo zaidi katika kutekeleza jukumu la kuisemea  Serikali hasa kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.


TAGCO na Idara ya Habari MAELEZO  Chachu Mageuzi Utendaji wa Maafisa Habari
Frank Mvungi- MAELEZO, Ruvuma

Moja ya Hatua zilizochukuliwa na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Seriklini (TAGCO) na Idara ya Habari (MAELEZO) ni kuweka utaratibu wa kufuatilia namna Maafisa Habari na Mawasiliano wanavyotoa taarifa za miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali  katika Mikoa na Halmashuri .

Akizungumzia jinsi Halmashuri ya Manispaa ya Songea inavyoweka mazingira wezeshi kwa Afisa Habari kutekeleza jukumu hilo, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bi. Tina Sekambo amesema kuwa dhamira yao ni kumpatia nyenzo zote muhimu katika kutekeleza majukumu yake ya kutoa taarifa za miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa manufaa ya wananchi na wamekuwa wakifanya hivyo kadiri rasilimali zinavyopatikana.

”Mimi natambua umuhimu wa kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu miradi ya maendeleo na katika hili Halmashuri yetu imeweka mkazo katika kumpatia vitendea kazi Afisa Habari wetu ili atekeleze jukumu la kutoa taarifa kwa wananchi" Alisisitiza Bi. Sekambo

Akifafanua amesema kuwa Halmashuri  hiyo itaendelea kuwekeza katika kuimarisha mfumo wa mawsiliano kati ya Serikali na wananchi kwa kutambua numuhimu wa suala hilo wamekuwa wakimshirikisha Afisa Habari katika kila jambo ili kumjengea uwezo katika kutoa taarifa kwa wananchi hasa za miradi ya maendeleo.

Naye Kiongozi wa ujumbe huo Bi Gaudensia Simwanza alisisitiza kuwa kuna umuhimu wa kuwaruhusu maafisa hao kushiriki katika mafunzo mbalimbali na kikao kazi ili kuwaongezea ujuzi katika kuisemea Serikali.

Ziara ya ujumbe huo imefanyika katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ikilenga kuhamasisha maafisa Habari kuongeza kasi katika kuisemea Serikali hasa kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ikiwa  inasisitiza utoaji wa huduma bora kwa wananchi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wakati na ikilenga kunufaisha wananchi wanyonge.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages