LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 30, 2018

RAIS DK. MAGUFULI ATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA SHEIKH WA MKOA WA MWANZA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Dk. John Pombe Mgufuli
Ikulu, Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeir bin Ally kufuatia kifo cha Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mwenyekiti wa Baraza la Ulamaa katika Mkoa huo Sheikh Salum Hassani Fereji kilichotokea usiku wa kuamkia tarehe 28 Julai, 2018 katika hospitali ya Bugando Mkoani humo.

Mhe. Rais Magufuli amesema anamkumbuka Sheikh Salum Hassani Fereji wa ucha Mungu wake, ukarimu, upendo kwa wananchi na namna alivyokuwa akiunga mkono juhudi za kudumisha amani na kusukuma mbele maendeleo.

"Nimesikitishwa sana na kifo cha Sheikh Fereji, nilipokuwa nikienda Mwanza alikuwa miongoni mwa viongozi wa dini waliokuja kunipokea na amekuwa akifanya kazi ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi makubwa na nchi yake, pole sana Mufti wa Tanzania na nakuomba unifikishie salamu zangu za pole kwa familia yake, Waislamu wote wa Mkoa wa Mwanza na nchi nzima pamoja na wote walioguswa na msiba huu" amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli amemuombea Marehemu Sheikh Salum Hassan Fereji apumzike mahali pema, Amina.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
30 Julai, 2018

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages