LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 1, 2018

RAIS DK. MAGUFULI AOMBOLEZA VIFO VYA WATU 20 WALIOKUFA KATIKA AJALI YA GARI MBEYA, LEO

Nimesikitishwa sana na taarifa ya ajali nyingine iliyotokea leo tarehe 01 Julai, 2018 katika mteremko wa Iwambi MkoaniMbeya na kusababisha vifo vya Watanzania wenzetu 20, hii ni ajali ya tatu kutokea Mbeya katika kipindi kifupi ambapo katikaajali hizo idadi ya Watanzania waliopoteza maisha imefikia 40.
Inauma sana kuwapoteza idadi hii kubwa ya Watanzania wenzetu katika ajali za barabarani ambazo tunaweza kuziepukaNawapa pole familiandugujamaamarafiki na wote walioguswa na vifo vya Watanzania wenzetu hawasote tuwaombeeMarehemu wapumzishwe mahali pema peponi na majeruhi wapone haraka
Ni salamu za rambirambi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MheDkt. John Pombe Magufuli alizozitoa leokupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw. Amos Makalla kufuatia ajali ya barabarani iliyosababisha watu 20 kufariki dunia nawengine 28 kujeruhiwa baada ya Lori (Semi-Trailerkuyagonga mabasi madogo ya abiria 3 likiwemo 1 lililolaliwa na tela lenyekontena baada ya kugongwa na kutumbukia mtoni katika eneo la IwambiMkoani Mbeya.
Katika ajali hiyo Lori lililokuwa limebeba kontena lenye shehena ya mzigolilikuwa linatokea Mbeya Mjini kwenda Tunduma(katika barabara ya Dar es Salaam – Tunduma – Zambiana mabasi madogo ya abiria (Daladalani yanayofanya safari zakekati Mwanjelwa na Mbalizi.
MheRais Magufuli amewataka viongozi wa Mkoa wa MbeyaJeshi la Polisi na Mamlaka nyingine zinazohusika katikaudhibiti wa usalama wa barabarani kujifakari na kuchukua hatua stahiki za kukabiliana na ajali hizo.
Haikubaliki hata kidogo kuendelea kupoteza roho za watu katika ajali tunazoweza kuzizuia amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages