Kiongozi Mwenza wa msafara kutoka Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari–MAELEZO, Bi. Gaudensia Simwanza (kushoto) akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu walipofanya ziara katika Halamashauri hiyo kuona utendaji kazi wa Maafisa Habari na Mawasiliano na namna wanavyokabiliana na changamoto mbalimbali katika kuisemea Serikali.
Mwakilishi
wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Casmir Ndambalilo akiagana na Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Bi. Changwa Mkwazu mara baada ya
ziara ya ujumbe kutoka Idara ya Habari-MAELEZO na Chama cha maafisa Habari na
Mawasiliano Serikalini (TAGCO).
(Picha zote na Idara ya Habari - MAELEZO)
Masasi Yajidhtiti Kuimarisha Mawasiliano na Wananchi
Na
Frank Mvungi- MAELEZO
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu, amesema
kuwa dhamira ya Halmashauri hiyo ni kuendelea kuimarisha mawasiliano na
wananchi ili waweze kufahamu miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na
Serikali.
Akizungumza
na ujumbe wa viongozi kutoka Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini
(TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO, uliomtembelea Ofisini kwake Bi. Mkwazu
amesema kuwa halmashuri hiyo inatambua umuhimu wa wananchi kupata taarifa za
miradi ya maendeleo kwa wakati kupitia vyombo vya habari.
“Afisa
Habari wetu anashiriki kikamilifu katika jukumu hili la kuwajulisha wananchi
kuhusu miradi ya maendeleo inayoteklezwa na mikakati yetu ni kumuwezesha zaidi
kadiri rasilimali zitakavyopatikana kwa kumpatia vitendea kazi bora ili atekeleze
jukumu hili kwa ufanisi, “alisisitiza Bi. Mkwazu
Mkurugenzi
huyo aliielezea sekta ya mawasiliano kama nyenzo muhimu katika kuwaletea
wananchi maendeleo kwa kuwa wanapata elimu kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo
kilimo.
Aliongeza
kuwa suala la mawasiliano katika Halmashauri hiyo ni limepewa kipaumbele kwa
kuwa ndiyo chachu ya maendeleona wananchi wanahitaji kufahamu mipango
mbalimbali ya maendeleo ya Halmashauri hiyo ili nao waweze kushiriki kikamilifu
katika kutekeleza mipango hiyo.
Kwa
upande wake kiongozi wa ujumbe huo Bi. Gaudensia Simwanza amesema kuwa ni
wakati muafaka kwa maafisa habari na mawasiliano Serikalini kuwa na mawasiliano
ya kimkakati na kuangalia namna bora ya kuwasiliana na wananchi kuhusu yale
yanayoteklezwa na Serikali katika maeneo yao.
“Ni
muhimu kwa Afisa Habari kuonesha umuhimu wa mawasiliano kwa kutekleza majukumu
yake kwa weledi” alisisitiza Simwanza.
Ziara
ya Viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na
Idara ya Habari-MAELEZO inalenga kuimarisha utendaji kazi wa Maafisa Habari na
Mawasiliano Serikalini katika Mikoa na Halmashuri hapa nchini.
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇