LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 5, 2018

MBUNGE STEPHEN NGONYANI 'MAJI MAREFU' AZIKWA KOROGWE, TANGA

Korogwe. Vilio, simanzi vimetawala leo Alhamisi Julai 5, 2018 katika mazishi ya aliyekuwa mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Steven Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu.

Wananchi waliozungumza na MCL Digital wamesema wamepoteza mtu muhimu kwa kuwa alikuwa anajua shida zao na amewasaidia katika masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na maeneo yao kupata maji ya uhakika pamoja na barabara zinazopitika muda wote.

“Alikuwa akitujali wananchi wake. Alikuwa tofauti na wengine waliomtangulia. Alihakikisha vijana hawasumbuliwi kabisa katika biashara zao, hasa wanaoendesha bodaboda na bajaji,” amesema Ayubu Richard, mkazi wa Korogwe ambaye pia ni dereva bodaboda.

Mariam Salimu mkazi wa kijiji cha Kwamndolwa alikozikwa Majimarefu leo jioni, amesema katika kijiji hicho kulikuwa na shida ya maji lakini kupitia mbunge huyo sasa maji yanapatikana, “hata barabara ipo na inapitika.”


Msemaji wa familia ya marehemu, Hilary Ngonyani amesema familia ilikuwa ikimtegemea kwa kiasi kikubwa.


“Kama tungetakiwa kuchanga fedha ili ndugu yetu asifariki dunia tusingesita kufanya hivyo. Ila ukweli unabaki palepale kuwa jambo hilo haliwezekani kwa kuwa kila mmoja atafariki,” amesema.


Viongozi mbalimbali wameshiriki ibada ya mazishi ya mbunge huyo akiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages