LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 24, 2018

ZIARA YA KINANA ZIMBABWE

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha  ZANU-PF cha Zimbabwe Dk. Obert Mpofu, Makao Makuu ya ZANU-PF Jijini Harare, jana. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana amefanya ziara ya kukitembelea chama cha ZANU-PF cha nchini Zimbabwe ikiwa ni mwendelezo wa utamaduni wa vyama hivyo kutembeleana ili kuimarisha na kuendeleza Uhusiano na Mshikamano wa kihistoria uliopo baina ya vya CCM na ZANU-PF, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti na Katibu Mkuu wa ZANU-PF. Katika ziara hiyo ameongozana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Dk. Edmund Mndolwa, Mwenyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka na Mwenyekiti wa UVCCM Kheri James
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahma Kinana akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Katibu Mkuu wa ZANU-PF, pamoja naye ni Wenyeviti wa Jumuiya za CCM na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe
Katibu Mkuu wa CCM akiwa na Katibu Mkuu wa ZANU-PF Ndugu Dk. Obert Mpofu ofisini kwake.
Katibu Mkuu wa CCM na Wenyeviti wa Jumuiya za CCM wakiwa katika picha ya pamoja na katibu Mkuu wa ZANU-PF. Kutoka kulia ni balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. Luteni Jenerali Charles Makakala, akifuatiwa na Ndugu  L. Matuke Mnadhimu na Katibu masuala ya Usalama ya ZANU-PF.
 Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkabidhi Rais wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa ZANU-PF  Emmerson Mnangagwa barua maalum kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli
 Mkuu wa CCM lAbdulrahman Kinana akmshukuru Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe na Mwenyekiti wa ZANU-PF Ndugu. Emmerson Mnangagwa baaada ya kumkabidhi barua maalum kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages