LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 20, 2017

MKUTANO WA KAMPENI NYUMBANI KWA MGOMBEA WA UDIWANI KATA YA KIJICHI WATIA FORA, MAMIA YA WATU WAFURIKA.

Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akimnadi mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Kijichi, Temeke Dar es Salaam, Eliasa Mtalawanje, uliofanyika jana katika eneo la nyumbani kwa mgombea huyo/
Kusilawe akimnadi mgombea huyo
Mgombea wa CCM katika uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi, Eliasa Mtalawanje, akinadi sera na kuomba kura kwa wananchi. Mtarawanje ameahidi kutengeneza mfumo bora utakaowaweka pamoja Kina mama na Vijana katika kubuni namna ya kujikwamua kiuchumi kwa njia wa kuunda vikundi kama vya Saccos na vikundi vingine vya uzalishaji mali. Pia amesema kama Diwani kijana atahakikisha anawatumikia wananchi kwa juhudi na maarifa kuthibitisha kuwa vijana wanapoaminiwa wanaweza.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamekaa juu ya kibaraza ili kuweza kmuona na kumsikia vizuri mgombea huyo
Mtarawanje akiwasalimu wananchi baada ya kuwasili mkutanoni
Katibu wa Siasa na Uenezi Wilaya ya Temeke akihamasisha wananchi kwenye mkutano huo
Vijana wa hamasa wakishangilia jambo
Katibu wa CCM mkoa wa Dar es  Salaam Saad Kusilawe akiwasili mkutanoni huku akisindikizwa Mwenyekiti mpya wa CCM Wilaya ya Temeke Almishi Hazal
Kijana akimwingiza mgombea wa Udiwani katika kata hiyo ya Kijichi kutoka chama kimoja cha siasa cha upinzani
Kijana akatoa kioja baada ya kutoa mfukoni kitambaa ya kufuta jasho, hirizi ikadondoka
Kijana akiishangaa hirizi hiyo
Eliasa akiteta jambo na Mkubwa na Wanawe
Vijana kutoka Ofisi Ndog ya Makao Makuu ya CCM Lumuba wakiwa kwenye mkutano huo kuongeza hamasa
Hawa pia ni vijana kutoka Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ofisi Ndogo ya Makao makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam
Baadhi ya viongozi wa meza kuu wakiwa kwenye mkutano huo
Baadhi ya viongozi na wana CCM wakiwa kwenye mkutano huo
Msanii akishirikiana na vijana wa hamasa kuhangamsha mkutano
Mwenyekiti  mpya wa Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Mafia Ndugu Al Abadawi, akitoa salam zake huku wananchi wakimsikiliza kwa makini kwenye mkutano huo
Ndugu Al Abadawi akifafanua jambo wakati akiendelea kuzungumza 
Ndugu Al Abadawi akizungumza kwa msisirizo mkubwa
Al Abadawi akisalimiana na Eliasa baada ya kutoka jukwaani
Katibu wa CCM Wilaya ya Temeke akizungumza
Meya wa Temeke Abdallah Chaurembo akisalimia wananchi kwenye mkutano huo, na kuzungumza kuhusu umuhimu wa wananchi kumchagua mgombea wa CCM Udiwani kata ya Kijichi.
Mbunge wa Mbagala Issa Mangungu, akisalimia wananchi kwenye mkutano huo, na kuzungumza kuhusu umuhimu wa wananchi kumchagua mgombea wa CCM Udiwani kata ya Kijichi.
Mwanachama mpya wa CCM aliyehamia kutoka ACT Wazalendo akipwa pongezi na mgombea Eliasa
Nyomi ya wananchi ikiwa kwenye mkutano huo
Elimeshi akizungumza kumkaribisha Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe
Kusilawe akiwa tayari jukwaani kwa mbwembwe
Mwananchi akiwa ameweka kandambili kwenye mkono huku ameshika bango la mgombea Eliasa
Mishi akionyesha kati alizobadhiwa na wananchama waliojiunga na CCM kutoka ACT kwenye mkutano huo
Mmoja wa waliokuwa wanachama wa ACT akizungumza baada ya kuhamia CCM kwenye mkutano huo
Akionyesha kadi yake ya ACT kabla ya kumkabidhi Mishi
Kisha akakabidhi kadi hiyo
Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akimuombea kura Eliasa
Mwananchi akiwa kwenye mkutano huo huku akiendelea na malezi
Mgombea Eliasa akimpongeza Ndugu Amina baada ya kuhamia CCM akitokea Chadema, wakati wa mkutano huo
Eliasa akimtambulisha Ndugu Amina kwa Mangungu
Wadau wakiwa imara kuhakikisha mkutano huo unaisha salama
Viajana wa hamasa wakipiga kwata kuchangamsha mkutano huo
Eliasa akipongezwa na Kusilawe baada ya hotuba yake nzuri jukwaani
Eliasa akiteta jambo na Mangungu kwenye mkutano huo
Kusilawe na viongozi wengine wakiongoka baada ya mkutano
Wananchi wakiwa bado wapo kwa wingi baada ya mkutano kumalizika
Eliasa akiagana na wazee maarufu baada ya mkutano huo
Wananchi wakaiwa wamesimama kwa shauku wakati Eliasa akiwa katika gari iliyombeba tayari kwa kuondoka eneo la mkutano huo

Hili ni tukio la mtu mmoja aliyeumia wakati wa purushani za kumuona mgombea, alianguka kwenye mtaro. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages