HABARI MPYA

Your Ad Spot

Aug 14, 2017

RAIS WA MISRI AWASILI NCHINI TANZANIA LEO

 Rais Dk.John Magufuli, akisalimiana na Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere  Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya siku mbili.
 Vikundi vya vya ngoma na Wananchi mbali mbali wakiwa katika Uwanja wa Ndege wa  Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam katika mapokezi ya Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi leo
 Kikundi cha Brass Bandi kikiburudisha wakati wa mapokezi ya Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi alipowasili leo katika Uwanja wa Ndege wa  Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya siku mbili
 Rais Dk.John Magufuli na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein wakiwapungia mikono wananchi waliofika katika mapokezi ya Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi, leo katika Uwanja wa Ndege wa  Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya siku mbili
 Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi akienda kukagua gwaride la rasmi baada ya kuwasili leo  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam
 Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi akifuatana na Makamanda wa Jeshi la Ulinzi JWTZ leo baada ya  kukagua gwaride rasmi  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbilI
 
 Rais wa Zanzinar Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi wakati wa  mapokezi  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam   nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kwa mualiko wa  Rais.Dk. John Magufuli
 Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa  wakiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam  wakati wa   mapokezi ya Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi leo
Rais Dk.John Magufuli, na mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi wakiondoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere baada ya mapokezi.
 Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi (katikati) na Ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na Viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakiongozwa na Rais Dk.John Magufuli, Ikulu ya Jijini Dar es Salaam, leo.
 Mazungumzo ya Viongozi baina ya Ujumbe wa Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi (kulia) na Viongozi wa Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais Abdel Sisi na Ujumbe wake wakiwa nchini kwa ziara ya siku mbili, (Picha na Ikulu).

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages