LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 1, 2017

MFUKO WA PSPF WAKABIDHI MASHUKA KWA WODI YA WATOTO HOSPITALI YA MNAZI MMOJA, ZANZIBAR

Maafisa wa Mfuko wa PSPF kulia Faidha Khatau na Hazina Konde wakimkabidhi mashukaka Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dr Ali Salum Ali anayefutia ni Mkurugenzi Utawala na Uendeshaji Dr. Abubakar Khamis Hamadi, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa jengo jipya wa Hospitali ya Watoto Mnazi mmoja PSPF imekabidhi mashuka 75 kwa ajili ya wodi za watoto katika hospitali hiyo Kuu Zanzibar ikiwa ni moja ya kusaidia Jamii.  
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar Dr. Ali Salum Ali akipokea mashuka kutoka kwa Maafisa wa Mfuko wa PSPF Tawi la Zanzibar Bi Hazina Konde (katikati) na Afisa Mkuu wa Tawi la Zanzibar PSPF Bi. Faidha Thatau wakikabidhi mashuka hayo kwa ajili ya matumizi ya Wodi ya Watoto katika hospitali ya Taifa ya Mnazi Mmoja Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika majengo mapya wa hospitali hiyo Zanzibar. 
Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa PSPF Tawi la Zanzibar Bi Faidha Thatau akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi mashuka kwa Uongozi wa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar. Mfuko wa PSPF hutowa huduma za mafao mbalimbali kwa Wanachama wake Bima ya Afya kwa wateja wao.  
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar Dr. Ali Salum Ali akitowa shukrani kwa Uongozi wa Mfuko wa PSPF kwa msaada wao huo na kuwataka isiwe mwisho iwe ni endelevu kwa kutoa misaada mbalimbali kwa hospitali hiyo uwezo ukiruhusu.
Afisa Mfawidhi wa Mfuko wa PSPF Bi. Faidha Khatau akigawa vipeperushi vya maelezo ya PSPF kwa viongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja kujuwa huduma zinazotolewa na Mfuko huo. 
Viongozi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja wakifuatilia vipeperushi vya Mfuko wa PSPF baada ya kukabidhiwa kupata maelezo ya PSPF, wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa mashuka kwa ajili ya Wodi ya Watoto Zanzibar.  
Afisa Mfawidhi Mfuko wa PSPF  Tawi la Zanzibar kulia Bi Faidha Khatau akimkabidhi mashuka Afisa Muunguzi katika Wodi ya Watoto Hospitali ya Mnazi Mmoja Bi. Fatma Ali Mzee na kushoto Afisa Mfawidhi Msaidizi Bi Hazina Konde, wakiwa katika moja ya Wodi ya Watoto katika hospitali mpya ya Watoto Mnazi Mmoja.  
Maafisa Wafawidhi wa PSPF Tawi la Zanzibar wakitandika kitanda katika moja ya vitanda katika Wodi ya Watoto Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar baada ya kukabidhi mashuka hayo 75 kwa ajili ya hospitali hiyo ya Watoto Zanzibar. 
Maafisa Wafawidhi wa PSPF Tawi la Zanzibar wakitandika kitanda katika moja ya vitanda katika Wodi ya Watoto Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar baada ya kukabidhi mashuka hayo 75 kwa ajili ya hospitali hiyo ya Watoto Zanzibar. 
Maafisa wa Mfuko wa PSPF Tawi la Zanzibar wakitoka katika jengo ya hospitali ya Watoto Mnazi Mmoja baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhi msaada wa mashuka kwa ajili ya matumizi ya Wodi ya Watoto Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar. Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com.
Email othmanmaulid@gmail.com Mobile.0777424152. 

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages