LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 30, 2017

JAFO AHIMIZA WANANCHI KUTUNZA MIRADI YA MAJI

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Rutala wilayani Ukerewe mkoani Mwanza juu ya utunzaji wa miradi ya maji.
--------------------
UKEREWE, MWANZA
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo amewataka wananchi wa wilaya ya Ukerewe kutunza miradi ya Maji kwa kuwa serikali inaigharamia kwa fedha nyingi.

Jafo aliyasema hayo alipotembelea mradi mkubwa wa maji wa Kazilamkanda ambao utahudumia vijiji vipatavyo 13 wilayani humo.

Amesema serikali inafanya jitihada za kuwatatulia wananchi wake kero mbalimbali ikiwemo ya upatikanaji wa huduma ya maji, hivyo ni vyema wakatunza miundombinu ya miradi hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Akikagua mradi huo, Jafo alimpongeza Mkandarasi aliye jenga chanzo na tanki la kuhifadhia maji la lita 680,000 ambaye ni Lutare Make Enginnering Ltd kwa kazi nzuri.

Amesisitiza kukamilishwa kwa usambazaji wa Maji katika vijiji vyote 13 kabla  ya Disemba 30 mwaka huu. 

Naibu Waziri huyo amesisitiza kulazwa mabomba yaliyo na ubora ili kuepusha kupasuka kwa mabomba endapo mabomba hayo yatakuwa hayana viwango na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi na halmashauri baada ya kukabidhiwa mradi husika.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akipata taarifa kuhusu miradi ya maji wilayani Ukerewe.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akipata taarifa kuhusu miradi ya maji wilayani Ukerewe.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa tenki la maji
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Selemani Jafo akifanya ukaguzi wa mashine za kusukumia maji.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages