LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 3, 2017

WENJE NA MASHA WAREJESHWA TENA KUGOMBEA UBUNGE EALA, NI KATIKA SITA WALIOTEULIWA TENA NA CHADEMA

Na Mwandishi Wetu
Baada ya kushindwa kukidhi vigezo katika hatua ya kwanza, Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) sasa imewateua wanachama wake sita kwenda kugombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa kupigiwa kura na Bunge la Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana usiku na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema Tumaini Makene walioteuliwa ni pamoja na Ezekiel Wenje na Lawrence Masha, na walioongezeka kufikisha idadi ya wagombea sita, ni Profesa Abdalla Safari, Salum Mwalimu, Josephine Lemoyan na Pamela Massay.

Taarifa imesem, wagombea hao, wamepatikana katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kilichofanyika jana mjini Zanzibar na kuazimia kuwateua wanachama wao hao kugombea Ubunge wa Afrika Mashariki (EALA)".

Ofisa habari wa Chadema,Tumaini Makene amesema baadhi ya mambo walioteuliwa watayakamilisha katika hatua zingine za uteuzi kwa mujibu wa taratibu na Kanuni za Bunge la Afrika Mashariki (EALA).

Awali Wenje na Masha waliteuliwa na Chadema kuwania Ubunge wa EALA, lakini wakapigwa kikumbo, kutokana na kukosa kura za kutosha katika uchaguzi wa kuwapata wabunge wa bunge la EALA, uliofanywa na Wabunge wa Bunge la Tanzania hivi karibuni mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages