LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 23, 2017

SIYANTEMI AKAGUA GHALA LA CHAKULA WILAYANI MONDULI

Katibu Tawala wa Wilaya ya Monduli Robert Siyantemi, Jumanne tarehe 23/05/2017 ametembelea ghala linalotumika kuhifadhi shehena ya mahindi ya serikali (kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula Kanda ya Arusha - NFRA). 

Katika ziara hiyo Komredi Siyantemi amezungumza na Maofisa wa NFRA na baadhi ya watendaji wa serikali na kuagiza kuwa, zoezi hilo la uuzaji mahindi ya serikali kwa bei elekezi kwenye maeneo yenye ongezeko la bei linapaswa kusimamiwa kikamilifu kwa kufuata taratibu na miongozo. Wakati huo huo, Komredi Siyantemi amekagua utekelezaji wa zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa, linaloendelea wilayani Monduli.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages