HABARI MPYA

Your Ad Spot

Apr 22, 2017

VURUGU ZAZUKA MKUTANO WA CUF DAR, WAANDISHI WA HABARI WAUMIZWA

Mwandishi akitokwa damu mkononi
Na Mwandishi Wetu

BAADHI ya waandishi wa habari na wanachama wa CUF wamejeruhiwa baada ya watu wanane, waliokuwa wamevalia ninja na kuvamia mkutano wa wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), mabibo jijini Dar es Salaam.


Vurugu hizo zimetokea leo, wakati wanachama wa CUF walipokuwa kwenye mkutano huo na waandishi wa habari katika Hoteli ya Viva jijini Dar Es Salaam.


Vurugi hizo zilizua taharuki kubwa kwa waandishi wa habari na wakazi wa eneo hilo ambapo walifanikiwa kumkamata mmoja wa watuhumiwa hao na kumkata mguu wa upande wa kulia.

Baadhi ya mashuhuda wanasema watu wasiojulikana walifika katika eneo hilo wakiwa wamefunika nyuso zao na vitambaa huku wakitumia silaha za jadi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na taarifa zaidi atatujuza baada ya kufika eneo la tukio
PICHA YA VIDEO>BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages