LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 23, 2017

WAZIRI MAHIGA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WATEULE NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) leo tarehe 22 Machi, 2017 amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi Wateule 7 wanaowakilisha nchi zao nchini kutoka Hungary, Belarus, Guinea, Botswana, Niger, Cyprus na Bangladesh. Pichani Balozi Mahiga akipokea nakala za hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Hungary nchini, Mhe. Laszlo Eduard Mathe mwenye makazi yake Nairobi, Kenya.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akipokea nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Belarus nchini, Mhe. Dmitry Kuptel mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa na Balozi Mteule wa Guinea nchini Mhe. Sidibe Fatoumata KABA mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia mara baada ya kupokea Nakala zake za Hati za Utambulisho.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Botswana nchini, Mhe. Lebonaamang Thanda Mokalake mwenye makazi yake Lusaka, Zambia.
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Mokalake mara baada ya kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin.
Mazungumzo yakiendelea kushoto ni Maafisa wa Ubalozi wa Botswana ambao waliambatana na Mhe. Mokalake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Niger nchini, Mhe. Adam Maiga ZAKAKARIAOU mwenye makazi yake Addis Ababa, Ethiopia. 
Waziri Mahiga akiagana na Mhe. ZAKAKARIAOU mara baada ya kuwasilisha Nakala za Utambulisho.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Cyprus nchini, Mhe. Andreas Panayiotou mwenye makazi yake Muscat, Oman.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Bangladesh nchini, Mhe. Meja Jenerali Abul Kalam Mohammad ahaumayun KABIR mwenye makazi yake Nairobi, Kenya. 
Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. KABIR.Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Grace Martin na kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Bangladesh ambaye aliambatana na Mhe. KABIR.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (kulia) akizungumza na Balozi Mteule wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Mahruqi alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika suala la Makao Makuu ya Serikali kuhamia Dodoma na namna Ofisi za Ubalozi huo zinavyoweza kutumia fursa hiyo kuwashauri wafanyabiashara wa Oman kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu pamoja na huduma nyingine za biashara ambazo bado hazijawa za uhakika katika mji huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bi. Zainab Angovi (kushoto) akiwa na Bi. Patricia Kiswaga, Afisa Mambo ya Nje.
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi Mlima akiagana na Balozi Al Mahruqi

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages