LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 1, 2017

NAIBU WAZIRI JAFO AKAGUA UJENZI WA MABWENI SHULE YA SEKONDARI MBOGA

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza katika ziara ya  Naibu Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jafo,alipotembelea Shule ya Sekondari ya Mboga kukagua ujenzi unaondelea shuleni hapo.
Mheshimiwa Naibu Waziri Suleiman Jaffo alitazama Ujenzi wa Maabara Tatu za Sayansi zinazojengwa , ujenzi wa madarasa mawili, Jiko la kisasa na Bwalo na Mwisho Hostel ambazo zitachukua wanafunzi 796
 Mbunge Kikwete akitoa maelezo juu ya ujenzi wa Hostel unavyoendelea kwa Naibu Waziri Jafo . 
Mbunge akimshukuru Naibu Waziri kwa kukagua ujenzi unaoendelea katika kshule ya Sekondari Mboga.
Naibu Waziri Jaffo akiwa na wenyeji wake wa pili upande wa kushoto ni  Mkuu wa Wilaya Bagamoyo Alhaj Majid Mwanga, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri Ndg Zikatimu  na wa tatu ni Naibu Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jafo na Mhehimiwa Mbunge Ridhiwani Kikwete wa walipokwenda kukagua ujenzi shule ya Sekondari ya Mboga
Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo akiingia kwenye kikao cha kuzungumza na wadau wa maendeleo na watumishi wa Halmashauri
Dada Mkuu wa shule ya Mboga sekondari wa kwanza kulia  kakizungumza neno kumshukuru Mbunge kwa msaada wa kuwatafutia Hostel na kukamilisha Maabara na kumuahidi kuwa watasoma kwa bidii ili asife moyo kusaidia elimu jimboni humo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages