LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 25, 2017

DKT KEBWE AONGOZA KIKAO CHA MAANDALIZI YA MAONESHO YA KILIMO

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe akizungumza wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki
Baadhi ya washiriki wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki wakifatilia kikao hicho kwa makini
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akisikiliza kwa makini wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Masharikikilichofanyika Mkoani Morogoro
Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe Godwin Gondwe akifatilia kwa makini kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki kilichofanyika Mkoani Morogoro, Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo
Mkuu wa Wilaya ya Muheza Hajat Mhandisi, Mwanasha Tumbo akichangia jambo wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe ameongoza kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki inayounganisha Mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Pwani na Morogoro.

Kikao hicho kilichokuwa na Agenda sita kimefanyika Katika Ukumbi wa JKT Nane Nane Manispaa ya Morogoro ambapo kwa kauli moja kimepitisha Agenda zote sita ikiwemo kupitia Taarifa ya Tathmini ya Maonesho ya Nane Nane 2016 sawia na Taarifa ya Maandalizi ya Maonesho ya Nane Nane ya mwaka 2017 ambayo Kitaifa yanayotaraji kufanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumza wakati Akifungua kikao hicho Dkt Kebwe ameitaka kamati inayoratibu shughuli hizo ya TASO kuweka wazi mapato na matumizi ya fedha wanazozipata kwani kufanya hivyo ni kujenga zaidi uaminifu kwa wananchi na kujihuisha kwa pamoja na wadau mbalimbali ili kukuza uchumi nchini kupitia Kilimo.

Dkt Kebwe alisema kuwa TASO kutofanya hivyo ni njia mojawapo ya kuzifanya Halmashauri zingine kutochangia kwa kuhofia fedha zao kutumika pasina weledi uliokusudiwa.

Sambamba na hayo pia amewasihi wadaiwa sugu kulipa madeni yao haraka iwezekanavyo kwani kufanya hivyo itaongeza ustawi na uimara wa Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo na hatimaye Kilele chake kuwa na Tija kwa jamii.

Dkt Kebwe amewapongeza wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya waliohudhuria katika kikao hicho ambapo alisema kuwa wanafanya kazi nzuri na kuonyesha ushirikiano imara katika Maandalizi hayo japo amesisitiza kuongezwa kwa jitihada za Maandalizi ili Maonesho hayo yawe na weledi na tija.

Sherehe za Maonesho ya Kilimo Nane Nane hufanyika kwa lengo la kuwakutanisha wakulima, wafugaji, na wavuvi kwa kuwaelimisha watazamaji na hasa wakulima, wafugaji na wavuvi kujifunza na kupata uzoefu wa teknolojia na mbinu zinazotumika kuongeza uzalishaji katika eneo la kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Katika Maonesho hayo mambo muhimu hutawala ikiwa ni pamoja na kuonyesha mazao mbalimbali sambamba na mifugo mbalimbali kwenye mabanda.

Akizungumza na Mtandao wa www.wazo-huru.blogspot.com Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amewapongeza viongozi wote kwa namna ambavyo wanashiriki kuandaa Maonesho hayo huku akisema kuwa pamoja na Halmashauri ya Ubungo kuwa mpya na inaanza kushiriki katika Maonesho hayo kwa Mara ya kwanza atahakikisha kuwa maonesho yanakuwa na tija katika mabanda yote yanayoendelea kuandaliwa na Maafisa Kilimo, Uvuvi na Mifugaji.

MD Kayombo alisema kuwa kupitia Maonesho ya Kilimo mwaka huu 2017 wananchi watapata fursa ya kujifunza mbinu za ufugaji kwa kutumia mabanda bora, Uchanganyaji wa vyakula vya mifugo na ulishaji, Teknolojia bora ya ufugaji wa samaki wengi katika eneo dogo, Utotoleshaji vifaranga kwa kutumia incubator ya kienyeji na kisasa, Uhamilishaji wa samaki na Ng'ombe na teknolojia Nyinginezo.

Akifunga kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa Kikao hicho alizitaja changamoto za maandilizi za Maonesho ya Kilimo kuwa ni pamoja na ucheleweshaji wa michango kutoka kwa wadau mbalimbali pamoja na kuchelewa kuthibitisha mialiko kwa wageni walioalikwa kutembelea Maonesho ya Kilimo Nane Nane.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages