LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 3, 2017

TIMU YA WANAHABARI IRINGA YAPIGWA JEKI NA MBUNGE RITTA KABATI

Mbunge  wa  viti  maalum  mkoa  wa  Iringa Ritta Kabati (CCM) akimkabidhi mwenyekiti wa waandishi wa habari mkoani Iringa moja ya jezi alizotoa kwa waandishi wa habari kwa ajili ya mechi mbalimbali za timu hiyo
 Mbunge  wa  viti  maalum  mkoa  wa  Iringa Ritta Kabati (CCM) ameipiga jeki timu ya wandishi wa habari mkoa wa Iringa kwa kuwapatia   jezi  seti  moja ,mpira na pesa taslim kiasi cha Tsh  50O,000 ili viwasaidie katika malengo yao ya kukipiga ligi daraja la kwanza .

Na Fredy Mgunda,Iringa
Mbunge  wa  viti  maalum  mkoa  wa  Iringa Ritta Kabati (CCM) ameipiga jeki timu ya wandishi wa habari mkoa wa Iringa kwa kuwapatia   jezi  seti  moja ,mpira na pesa taslim kiasi cha Tsh  50O,000 ili viwasaidie katika malengo yao ya kukipiga ligi daraja la kwanza .

 Akikabidhi  msaada  huo kwa mwenyekiti wa chama cha wandishi wa habari mkoa wa Iringa Frank Leonard juzi    mbunge huyo alisema kuwa  yeye kama mlezi  wa timu hiyo ameamu kujingiza kwa miguu yote kuisaidi timu hiyo ambayo inaonekana kufanya vema kwenye mchezo wa soka mkoani hapo .

Kabati alisema kuwa licha ya kuwa mpira ni ajira pia unamsaidia mtu kuwa na afya njema itakayomsaidia kujiepusha na magonjwa yanayoepukika ikiwemo presha .
“Niwatie moyo hichi mulichokianzisha ni kizuri na timu yenu ina fanya vizuri na juzi tu mumenyakua kombe la Spanest  kwa kuwanyuka kitisi huu ni ushahidi tosha mukiendelea hivi hivi mutakuja kuingia ligi daraja la kwanza na baadaye ligi kuu .

Kabati  aliwataka   wadau  wengine mkoa  Iringa na nje ya  Iringa  kuendelea  kujitolea  kuisaidia   timu   hiyo    ya wanahabari ili iendele kufanya vema ndani na nje ya mkoa wa iringa

Akipokea vifaa hivyo mwenyekiti wa wanahabari mkoa wa Iringa Frank Leonard alimshukuru mbunge huyo kwa vifaa na fedha alizotoa huku akimuahidi mbunge huyo kuwa timu hiyo itakipiga na timu mbalimbali ikiwemo timu ya bunge la jamuhuri wa muungano wa Tanzania

Frank alisema kuwa timu hiyo imekuwa ikifanya vema kutokana na kuwa na wandishi wazuri vijana waliona ari ya kusakata kambumbi hivyo ni vema timu ya bunge kujipanga kisawasa kwani hawata toka salama pindi watakapokipiga nao mjini dodoma

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages