HABARI MPYA

Your Ad Spot

Feb 25, 2017

AMSCO YAWAKUTANISHA VIONGOZI WA MASHIRIKA NA TAASISI KUJADILI UMUHIMU WA MAFUNZO NA UJUZI KATIKA KUKUZA UCHUMI

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Anne S. Makinda akizungumza kwenye mkutano uliowakutanisha viongozi wa mashirika na taasisi ili kujadili ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' ambao umeandaliwa na kampuni ya African Management Services (AMSCO) ukiwa na lengo la kujadili umuhimu wa mafunzo kwa rasilimali watu katika kukuza uchumi.(Picha na Geofrey Adroph)
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde akizungumza kuhusu upatikanaji wa ajira katika nyanja mbalimbali hasa pale ukuaji wa uchumi unapoimarika wakati wa kujadili ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' ambao uliwakutanisha dawau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya ATMS, Balozi Jan Berteling akizungumza jambo kwenye mkutano huo uliowakutanisha viongozi wa mashirika na taasisi kuhusu ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Recency jijini Dar.
Meneja wa Heineken Afrika Mashariki na Kati, Kayode Adeuja akizungumzia jinsi kufanya biashara na kukuza mtani kama kampuni hiyo ilivyoimarika wakati wa kujadili ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Recency jijini Dar.
Mwezeshaji wa Majadiliano Bi. Catherinerose Barreto(aliyesimama) akitolea ufafanuzi moja ya jambo lililokuwa likijadiliwa katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Hotel ya Hyatt Recency jijini Dar
Baadhi ya wadau wakichangia mada kwenye majadiliano
  Mwenyekiti wa AMSC, Ali Mufuruki akizungumza na waandishi wa habari walivyowakutanisha viongozi wa mashirika na taasisi ili kujadili  uuhusu ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference'
Baadhi ya viongozi wa mashirika na taasisi mbalimbali wakifuatilia majadiliano kuhusu ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' kwenye ukumbi wa Hyatt Recency jijini Dar

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Anna Makinda amesema ukuaji wa uchumi hauwezi kufikiwa endapo hakutakuwa na uwekezaji wa kutosha katika mafunzo kwa rasilimali watu.

Mama Makinda ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa kujadili ukuaji wa uchumi 'Business Transforming Africa Conference' ambao umeandaliwa na kampuni ya African Management Services (AMSCO) ukiwa na lengo la kujadili umuhimu wa mafunzo kwa rasilimali watu katika kukuza uchumi.

Amesema hakuna usawa kati ya ujuzi unaotolewa mashuleni na mahitaji ya soko la ajira jambo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa ukosefu wa ajira kwa wahitimu wengi ambao hushindwa kukidhi mahitaji ya soko la ajira.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde alisema kuwa  pamoja na jitihada zinazofanywa na wadau wote wanaoshiriki katika kukuza uchumi ni muhimu kwa wadau hao kwenda sambamba na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano ili kuweza kufikia malengo ya pamoja yaliyokusudiwa.

AMSCO imekuwa ikiandaa mikutano ya namna hii kwa lengo la kukuza uchumi wa taasisi, mashirika nchi kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages