LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 5, 2016

NUKUU ZA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI


Image result for picha ya magufuli
RAIS JOHN POMBE MAGUFULI
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli ni aina ya kiongozi ambaye watanzania tulikuwa tunamsubiri kwa muda mrefu, kwa kawaida kila anapohutubia kwenye mikutano na sehemu yoyote huwa anaacha gumzo kutokana na kauli zake ambazo anazitoa na kusababisha watu kucheka na wengine  kununa.

Kwenye mtandao huu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),  ninawaletea kipengele kipya kinachoitwa Nukuu za rais, John Pombe Magufuli ambacho kitaangazia maneno yote yenye kuleta furaha kwa wapenda maendeleo na huzuni kwa wapinga maendeleo.
  
NUKUU:
  
"Ukigombea mwaka wa kwanza ukashindwa, mwingine ukashindwa, mwingine ukashindwa, huwezi kujifunza hata kwenda kuuza nyanya sokoni kwamba biashara hii imekataa kwako,”. 

MAANA YAKE









Unapogombea uongozi na kushindwa zaidi ya mara moja, wapishe na wengine wagombee.




Rais ametoa kauli hiyo siku ya Jmamosi, 3/4/2016 wakati akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kisiwani Unguja ambako alikwenda kushukuru wananchi kwa kumchagua kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka 2015. 
Mawasiliano ya aliyeandika nukuu hii ni 0713 311 300



No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages