LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 8, 2016

MASWALI NA MAJIBU BUNGENI LEO


Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzania na Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe (MB) akimuuliza swali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) kuhusu hali ya uchumi nchini ambapo Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa alimhakikishia kuwa Serikali ipo imara katika kusimamia ipasavyo uchumi wa nchi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akijibu maswali ya wabunge wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akisalimiana na Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzania Bungeni na Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe (MB) wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akiwashukuru wabunge mara baada ya kumaliza kujibu maswali wakati wa kikao cha tatu cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Leo Mjini Dodoma.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na raia katika kuhakikisha inakabiliana na biashara haramu ya Madawa ya Kulevya. 
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akijibu swali bungeni ambapo alisema ambapo alisema Serikali imetenga shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuboresha Magereza ya watoto pamoja na makao ya Wazee nchini. 
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba akijibu swali bungeni ambapo alisema serikali ipo katika mazungumzo na serikali ya China kwa ajili ya kuboresha zao la Tumbaku.
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni akijibu swali bungeni ambapo alisema Wizara imetenga Shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kuboresha hali ya Magereza nchini.


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongea na wabunge na kuviasa vyama vya siasa vyenye tabia ya kufukuza wabunge kuacha hivyo kwani hatuwatendei haki wapiga kura na ni gharama kwa serikali. Picha na Hassan Silayo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages