LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 11, 2016

KINANA AKUTANA NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA CHA MPLA YA ANGOLA.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndg Abdulrahman Kinana akiongozana na Katibu wa Halmashauri Kuu, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Pindi Chana wamekutana na high level delegation kutoka Chama cha MPLA cha Angola kujadili namna bora ya kuimarisha uhusiano wa vyama hivyo viwili na kufungua ushirikiano baina ya malada wake kwa fursa za mafunzo na itikadi.

MPLA na CCM ni miongoni mwa vyama sita (6) vya nchi za kusini mwa Afrika ambavyo vilishirikiana katika kupambana na ukoloni na vimeendelea kushirikiana kama vyama rafiki (sisters party).

Vyama hivyo chini ya uongozi wa CCM vinategemea kujenga chuo kikuu kikubwa nchini Tanzania kwa ajili ya mafunzo kwa makada wa vyama hivyo juu ya itikadi, uenezi, ujasiriamali na uongozi.

IMG-20160910-WA0215.jpg

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages