LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 18, 2016

RAIS DK. MAGUFULI AMTEUA MRISHPO GAMBO KUWA MKUU MPYA WA MKOA WA ARUSHA

MRISHO GAMBO
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya uongozi na kumteua Mrisho Gambo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuanzia leo, Alhamisi, Agosti 18,2016.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Gambo anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Felix Kijiko Ntibenda ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Amesema Ntibenda anahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu ambako atapangiwa majukumu mengine.

Kabla ya uteuzi huo, Gambo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha. Ataapishwa kesho, Ijumaa, Agosti 19, 2016, saa 3 asubuhi, Ikulu jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages