SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Chama Cha Mapinduzi (CCM)
kimepokea kwa majonzi na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Aboud Jumbe
Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kilichotokea jana tarehe 14th Agosti 2016 nyumbani kwake
Mji Mwema, Kigamboni jijini Dar es
salaam.
Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, alikuwa
Makamu Mwenyekiti wa Kwanza wa Chama cha Mapinduzi mara baada ya kuunganisha
Chama cha ASP na TANU.
Mzee Jumbe alikuwa ni
Kiongozi mchapakazi, Muasisi na Mwanamapinduzi aliyeshiriki katika harakati za
ukombozi wa Zanzibar, ametoa mchango mkubwa katika kuunganisha vyama vya TANU
na ASP. Ameweka rekodi nzuri ya kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania aliyetumikia nafasi hiyo kwa muda mrefu (1972 – 1984) na kutembelea
Vijiji na Wilaya nyingi za Tanzania Bara na Zanzibar na kusikiliza kero na
changamoto za wananchi.
Aidha, Katibu Mkuu wa CCM
Ndg Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe Ali Mohamed Shein, familia ya Mzee Aboud
Jumbe pamoja na Wazanzibari wote kufuatia kifo cha Kiongozi wetu. Tunaungana
nao katika msiba huu ambao pia ni msiba wetu.
WanaCCM nchi nzima
tunamuomba Mwenyezi Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Mzee Aboud Jumbe
Mwinyi. Amina
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇