LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 12, 2016

TANZANIA: USHIRIKIANO BADO UNAHITAJIKA KUUKABILI UGONJWA WA UKIMWI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
  Jinsia,Wazee na Watoto,DK.Hamisi Kigwangalla
 akizungumza katika mkutano wa
 Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa
 kuhusu ukimwi unaoendelea
 hapa Umoja wa Mataifa,
Na Mwandishi Maalum, New York
Mkutano wa nganzi ya juu  kuhusu  ukimwi jana  ( alhamis) uliingia katika  siku yake ya pili ambapo viongozi mbalimbali wakiwamo  Mawaziri na  Naibu waziri  wanaohusika na masuala ya afya wameendelea kuelezea nini ambacho  nchi zao zinatekeleza  katika kukabili na kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vinavyo sababisha ukimwi  pamoja na  huduma   wanazopatiwa  watu ambao wamekwisha kuathirika na kuugua.

 Mmoja ya  nchi ambayo iliwasilisha   mafanikio,  changamoto na mwelekeo  wa baadaye katika kukabiliana na  janga  la ugonjwa wa ukimwi,  ugonjwa ambao  jumuiya ya kimataifa umejiweka lengo la  kuutokomeza ifikapo mwaka 2030 ili  kuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Juhudi za Tanzania dhidi ya Ukimwi,   zilielezwa  na    Naibu Waziri wa Afya,  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Mhe. Dr. Hamis A Kigwangalla (Mb). Ambaye  katika  maelelezo yake, amesema,  Tanzania inaamini   kuwa   inawezekana  kufikia hali ya  kutokuwa na  maambukizi mapya, kumaliza  ubaguzi na  unyanyapaa, na kuwa na kiwago sifuri   cha vifo   vinavyohusiana na  ukimwi fikapo mwaka 2030.

Hata hivyo anasema,  ili kufikia  hatua  hiyo au mafanikio hayo,  mambo   kadhaa yanapashwa kufanyika,  yakiwamo ya  uimarishwaji wa elimu ya kinga,  vijana na   jumuiya kwa ujumla kufundishwa mbinu  za kuepukana na tabia hatarishi ambazo zinachangia ongozeko la  waathirika na kuhakikisha  upatikanaji  kirahisi wa za dawa  na ambazo zitakuwa  za gharama nafuu.

Kwa mujibu wa  Naibu  Waziri ambaye anaongoza ujumbe wa Tanzania katika  mkutano  huu, amekwenda mbali  zaidi   kwa  kusema  pia patahitajika kupunguza vifo vitokanavyo na   ugonjwa wa Kifua Kikuu kwa watu wanaoishi na  virusi vya ukimwi,  kujadili   masuala ya jinsia  pamoja na  mila na tamaduni,  kutenga raslimali za kutosha kwaajili ya   watu wenye mahitaji wakiwamo vijana, kuwa na   viwanda  vitakavyoweza kuzalisha dawa.

Akizungumza baadhi ya mafanikio ambayo Tanzania imekwisha kuyafikia katika kukabili tatizo la   ukimwi, Naibu Waziri  ameyataja baadhi ya mafanikio hayo kuwa ni   pamoja  na  kupunguza maambukizi mapya kutoka  140,000 mwaka 1990 hadi kufikia 63,000 mwaka 2014. Vile vile vifo vitokanavyo au vinavyosaabishwa na ukimwi pia  vimepungua kwa asilimi 40 katika kipindi hicho.
Akaeleza pia kwamba hata  watu wanaopatiwa huduma ya  matibabu nayo imeongezeka kufikia asilimia 60 huku  ongezeko likiwa kwa watoto  na hasa baada ya  kupitisha mpango   unaotambulika kama Option B+  miaka sita iliyopita.

Kuhusu kupungua kwa  raslimali fedha hususani kutoka kwa  wafadhili, Dr. Kingwangalla, amesema  katika  kukabiliana na changamoto hiyo, na  kwa kuzingatia wito wa jumuiya ya kimataifa kupanua wigo wa mapato ya ndani,  serikali ya Tanzania ilianzisha  Mfuko wa ukimwi,  (AIDS Trust Fund) mfuko anaosema hadi sasa  serikali ndiyo imekuwa mchangiaji mkuu, ingawa pia  kwamba sekta binafsi nayo inatazamiwa  kuchangia.

 Akasema sehemu  au nusu ya fedha hizo (55%) itakwenda kusaidia upatikanaji wa huduma na kuongeza kuwa juhudi hizo za serikali pia zimesaidiwa na  ushirikiano  baina ya Tanzania na  nchi nyingine  rafiki pamoja na mashirika ya kimataifa na akatumia fursa hiyo kuwashukuru wale  wote ambao wanachangia juhudi za serikali.

 Kuhusu  mipango  mingine ambayo  serikali  inaendelea nayo ,  Naibu waziri alikuwa na haya ya kueleza “ baada ya  kuwa tumeanza utaratibu wa kupima na kutibu kwa baadhi ya wilaya chache nchini, tunakusudia  kuisambaza huduma hiyo lakini   itakuwa  ni kwa hatua ili  kutoa nafasi ya kuwajengea uwezo watoaji wa huduma  ya afya, kuhuisha  mifumo ya usambazaji wa  vifaa  ikiwa ni  pamoja ushiriki wa  jamii   ili  iweze kupokea na kuukubali mfumo huu mpya wa utoaji wa huduma” ameeleza Naibu Waziri.

Akasisitiza zaidi kwa kusema ingawa  ugonjwa wa ukimwi  umeendelea kuwa  changamoto kubwa kwa maendeleo ya nchi  ambapo  inakadiriwa watu 1.5 milioni wameathirika, huku mzingo mkubwa ukiwaelemea wanawake na vijana hasa  watoto wa kike,  serikali ya  tanzania  itaendelea na jitihada zake za kuhakikisha inafikia lengo  la kutokuwa na maambukizi mapya,  kutokomeza unyanyapaa na ubaguzi, na vifo vinatokanavyo na ukimwi.

Katika hatua nyingine amesema ili kutorudisha nyuma mafanikio ambayo  Tanzania imeyafikia hadi sasa pamoja na  nchi nyingine kusini mwa Jangwa la Sahara  Jumuiya ya  Kimataifa inaombwa kusaidia jitihada zinazofanywa na serikali  za nchi hizo  za kuwa na  mapato yake yenyewe ya kugharamia   huduma za afya kwa wagonjwa wa ukimwi  na  pamoja na huduma nyinginezo badala ya kuziachia  kabisa jukumu hilo.


No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages