LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 17, 2016

PANAFRICAN ENERGY TANZANIA YAKABIDHI MADAWATI 800 KWA WILAYA YA KILWA


Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za kijamii wa Kampuni ya Uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy (CSR Manager) Andrew Kashangaki akifafanua jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya madawati kwaajili ya watoto wa shule za msingi wilayani Kilwa
Baadhi ya madawati yaliyotolewa na Kampuni ya uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy
Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za kijamii wa Kampuni ya Uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy (CSR Manager) Andrew Kashangaki(kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilay ya Kilwa Juma A. Njwayo madawati kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi wilayani mwake. Wanaoshuhudia ni baadhi ya viongozi wa halmashauri ya Kilwa, viongozi kutoka PanAfrican Energy na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Masoko katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Kilwa Masoko.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mh. Juma Abdallah Njwayo akiwaasa wanafunzi wa shule ya Msingi Masoko ambao ni moja ya wanufaikaji wa madawati 800 kutoka PanAfrican Energy kuyatunza madawati waliyopewa na kusoma kwa bidii.
Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za kijamii wa Kampuni ya Uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy (CSR Manager) Andrew Kashangaki akitoa neno wakati akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mh. Juma A. Njwayo madawati 800 yatakayosaidia watoto 2400 na kupunguza tatizo la uhaba wa madawati.
Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za kijamii wa Kampuni ya Uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy (CSR Manager) Andrew Kashangaki akitoa neno wakati akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mh. Juma A. Njwayo madawati 800 yatakayosaidia watoto 2400 na kupunguza tatizo la uhaba wa madawati.




PANAFRICAN ENERGY TANZANIA YATOA MADAWATI 800 KWA WILAYA YA KILWA 



 Kapuni ya uchimbaji gesi asilia PanAfrican Energy jana imekabidhi madawati 800 kwa ajili ya shule za msingi wilayani Kilwa yenye thamani ya shilingi za kitanzania Milioni 104. Makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Masoko iliyopo wilayani humo katika hafla fupi iliyoandaliwa na Kampuni hiyo, huku ikishuhudiwa na wana habari, viongozi mbali mbali wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Juma Njwayo, walimu, wanafunzi na wananchi wa Kilwa Masoko. Msaada huo wa madawati kwa ajili ya wanafunzi wa shule za Msingi ni kuunga mkono Kampeni ya uchangiaji madawati iliyoanzishwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli. 

Akiongea wakati akipokea madawati hayo Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mh. Juma Njwayo, ambaye alikua mgeni rasmi katika hafla hiyo aliwashukuru sana Kampuni ya PanAfrican Energy kwa msaada wao mkubwa wanaotoa kwa wilaya ya Kilwa. 

“Kwa niaba ya wana Kilwa naomba kutoa shukrani zetu za dhati kabisa kwa PanAfrican Energy kwa siku zote kutuangalia kwa jicho la tatu kwa mmekua mkijitoa kawa hali na mali kuwezesha huduma mbali mbali katika Wilaya yangu Ya Kilwa. Leo napokea madawati 800 ambayo yatasaidia kupunguza uhaba wa madawati mashuleni kwani yatasaidia watoto 2400 kutokukaa chini, hili si jambo dogo kabisa hivyo mnahitaji pongezi. 


Natoa wito kwa wadau wengine kuiga mfano huu walionesha PanAfrican Energy kwani bado tuna uhaba wa madawati katika shule zetu za msingi hapa Kilwa. Hapa katika Shule ya Msingi Masoko watapata madawati 145 ambayo yapo mbele yetu hapa na mengine 655 yaliyobakia yatagawiwa kwa shule zingine zenye uhaba huo. Tunategemea ifikapo katikati ya mwezi Julai tutakua tumemaliza tatizo la madawati katika shule za msingi wilayani humu. Pia alitoa wito kwa wanafunzi kutunza madawati hayo ili yaweze kunufaisha wanafunzi wengi zaidi.” 


“Mbali na kupata madawati pia tunawapongeza kwa kuwa na uzalendo na wilaya yetu kwani hata mzabuni aliyepata kazi ya kutengeneza madawati haya ni mwananchi wa Kilwa ambapo vijana kadhaa wamepata ajira kupitia kazi hiyo na kuongeza kipato chao. 


Ukiachilia mbali swala la elimu Kampuni hii imekua mstari wa mbele katika swala la afya pia ambapo katika kuupunguza vifo vya kina mama na watoto wanatujengea jengo la Mama Ngojea katika hospitali yetu ya Wilaya ambako kabla yam waka huu kuisha tutakua tumeshakabidhiwa jengo hilo pia wanakarabati kituo cha afya cha Kilwa Masoko.” Aliongeza Mh. Njwayo. 


Naye Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za jamii wa Kampuni ya Uchimbaji wa Gesi ya PanAfrican Energy Andrew Kashangaki alisema, “Ni furaha yetu kuona watoto wa kitanzania wanasoma kwa Amani bila kuwa na matatizo yeyote na ndomana tumesukumwa kuunga mkono sekta ya elimu nchini kwa kuanza na wilaya ya Kilwa. 


Leo tunakabidhi madawati 800 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilwa yatakayosaidia kupunguza tatizo la watoto wetu kukaa chini na wadawati haya yatagawanywa kwa shule za msingi mbalimbali kutokana na uhitaji wao. Sisi kama wadau wa Elimu tumefanya kile tulichoweza kufanya hivyo tunaamini kwa madawati haya tunawawezesha watoto wa kitanzania watakaosomea katika shule hizo kutoa ujinga na tunatengeneza Taifa la wasomi. 


Aliongeza kwa kusema kuwa, “Tayari tuna programu ya kusomesha watoto kutoka kisiwa cha Songosongo ambako kila mwaka tunasomesha watoto 28, tumejenga mabweni kwaajili ya watoto wa kike kisiwani songosongo, pia ujenzi wa maabara za kisasa kwa ajili ya masomo ya sayansi kwa shule za Sekondari hiyo yote ni kuhakikisha tunaweka mazingira mazuri ya kusomea kwa watoto wetu.” 

Wilaya ya Kilwa ilikua ina uhaba mkubwa wa madawati tangu mwaka jana lakini inaaminika kuwa ifikapo katikati ya mwezi Julai watakua wameshatatua tatizo hilo. Wamepata madawati kutoka kwa wadau mbalimbali ikiwemo Kampuni ya Uchimbaji gesi ya PanAfrican Energy iliyotoa madawati mengi zaidi yaw engine, huu ni mfano wa kuigwa kwa wadau wengine kwani mtoto wa mwenzako ni wako na kila mtoto ana haki ya kusoma katika mazingira rafiki.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages