LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

May 31, 2016

MWENGE WA UHURU WAMULIKA MAJIMBO MAWILI YA LINDI VIJIJINI


 Mwenge wa Uhuru ukiwasili kwenye uwanja wa mpira wa Mchinga I,wilaya ya Lindi vijijini ambapo ulizindua miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika Majimbo mawili wa wilaya hiyo, jimbo la Mchinga na jimbo la Mtama.
 Viongozi mbali mbali wakiwa wamesimama tayari kuupokea Mwenge wa Uhuru katika wilaya ya Lindi Vijijini
 Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Bw. George Jackson kitaifa akizindua mradi wa maji katika shule ya msingi Mchinga I.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Yahaya Nawanda wakiwaongoza waongoza Mwenge wa Uhuru kitaifa kupita juu ya daraja lililofunguliwa rasmi na kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Daraja hili linawaunganisha wakazi wa Mchinga II na Mchinga I.
 Wanafunzi wa shule ya sekondari ya kata ya Mnonela wakihushuhudia Mwenge wa Uhuru kwa kuushika ulipowasili shuleni hapo jimbo la Mtama , Lindi Vijijini.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kushoto) , mkimbiza Mwenge Kitaifa na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Yahaya Nawanda wakiwa wamekalia moja ya madawati 50 yaliokabidhiwa kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi  Mnolela.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akitoa heshima kwa Mwenge wa Uhuru kwenye viwanja vya shule ya msingi Madangwa.

Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Madangwa waliojitokeza kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru ambapo aliwaambia kuwa utekelezaji wa yale aliyoahidi umeanza na kuwahakikishia wananchi wa jimbo lake ahadi zake zitakamilika mapema zaidi.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages