HABARI MPYA

Your Ad Spot

May 25, 2016

KUTOKA BUNGENI LEO

 Mbunge wa jimbo la Nkasi Kaskazini (CCM) Mhe. Allya Kessy akizungumza jambo na Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Mhe. Halima Mdee nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo.
 Mwekekezaji na Msambazaji wa nguzo za umeme nchini kutoka Kampuni ya New Forest iliyoko mkoani Iringa akiwaonesha jambo Mbunge wa Nkasi Kaskazini Mhe. Ally Kessy (kushoto) na Mbunge wa jimbo laKilolo Mhe. Venance Mwamoto kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jummanne Maghembe (kushoto) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mhandisi Ramo Makani waifuatilia hoja mbalimbali za wabunge wakati wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo Bungeni Dodoma.
  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jummanne Maghembe (kushoto) na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mhandisi Ramo Makani waifuatilia michango mbalimbali ya wabunge wakati wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo Bungeni Dodoma.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Hussein Mwinyi akifuatilia kwa makini mjadala wa Waheshimiwa Wabunge wakati wa kipindi cha maswali na Majibu.
 Mbunge wa Bunda Mjini Mhe. Esther Bulaya akichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo
 Mwenyekiti wa Bunge ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Magharibi Mhe. Andrew Chenge akiongoza kikao cha Bunge leo mjini Dodoma.
Baadhi ya Wananchi kutoka jamii ya Wafugaji waliohudhuria kikao cha Bunge leo mjini Dodoma kushuhudia Michango ya Wabunge wakati wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma leo.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Hamis Kigwangala akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Bunge Bw. Owen Mwandumbya (kulia) na Mwandishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bw. Elisha Eliya leo mjini Dodoma.Picha/Aron Msigwa - MAELEZO
  

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages