LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 4, 2016

KINANA ASHIRIKI KUPAKA RANGI JENGO LA OFISI YA CCM MKOA WA SINGIDA AKUTANA NA WAJASIRIAMALI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi za CCM mkoa wa Singida ambapo alipokea taarifa ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM pamoja na kushiriki kupaka rangi ofisi za CCM mkoa wa Singida.
Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Singida Mary Maziku (kushoto)akisoma taarifa ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM  kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana .
 Wajumbe wa Kamati ya Siasa CCM mkoa wakisikiliza wakati Kaimu Katibu wa Mkoa Ndugu Mary Maziku akiwakilisha taarifa za maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye ofisi za CCM mkoa wa Singida.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Singida mara baada ya kupokea taarifa za maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Singida mara baada ya kupokea taarifa za maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupaka rangi jengo la  CCM mkoa wa Singida ikiwa sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Singida mjini Mwalimu Mussa Ramadhan Sima akishiriki kupaka rangi pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana jengo la ofisi za CCM mkoa wa Singida ikiwa sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 39 ambayo kitaifa yanafanyika mkoani humo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdul Rahman Kinana akishiriki ujenzi wa maabara ya shule ya Sekondari ya Unyianga iliyopo kata ya Unyianga mkoani Singida.
 Mbunge wa Jimbo la Singida mjini Mwalimu Mussa Suleiman Sima  akishiriki ujenzi wa maabara ya shule ya Sekondari ya Unyianga iliyopo kata ya Unyianga mkoani Singida.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdul Rahman Kinana akizungumza na wananchi wa kata ya Unyianga mara baada ya kushiriki ujenzi wa maabara ya shule ya Sekondari ya Unyianga iliyopo kata ya Unyianga mkoani Singida
 Mkurugenzi wa Manispaa ya mji wa Singida Ndugu Joseph Mchina akizungumzia mipango ya serikali ya kuharakisha kusajiliwa kwa shule ya sekondari ya kata ya Unyianga.
  Mbunge wa Jimbo la Singida mjini Mwalimu Mussa Suleiman Sima  akizungumza na wananchi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kushiriki ujenzi wa maabara ya shule ya Sekondari ya Unyianga iliyopo kata ya Unyianga mkoani Singida.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na diwani wa kata ya Unyianga Ndugu Geofrey Mdama mara baada ya kushiriki ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari ya kata ya Unyianga.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na mkulima wa zao la mtama Ndugu Elisha Mdaa wa kata ya Mtamaa pamoja na mbunge wa jimbo la Singida  Mwalimu Mussa Suleiman Sima kwenye shmaba la mkulima huyo ambapo pia alishiriki parizi.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki parizi kwenye shamba la mtama lililopo kata ya Mtamaa.

 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki parizi kwa kutumia jembe linalovutwa na ng'ombe maarufu kama plau kwenye shamba la mtama lililopo kata ya Mtamaa.
  Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mara baada ya kushiriki parizi kwa kutumia jembe linalovutwa na ng'ombe maarufu kama plau kwenye shamba la mtama lililopo kata ya Mtamaa mkoani Singida.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa wa Singida tayari kuzungumza na wajasiriamali.
 Mwenyekiti wa Wajasiriamali wa Singida mjini Ndugu Yahya Ally Mkhofoi akisoma taarifa yao kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajasiriamali wa Singida mjini ambapo aliwaeleza kuwa wanatakiwa kuwa na viongozi makini ambao wataweza kuwakilisha vizuri pia aliwataka viongozi kuwa karibu na wananchi wao.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati akizungumza na wajasiriamali wa Singida mjini.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Afisa Biashara wa Manispaa ya Singida Ndugu Erick Sinkwembe wakati akitoa ufafanuzi juu ya taratibu za kupata leseni za usafirishaji wa abiria kwa boda boda zinazotolewa na SUMATRA.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages