LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 8, 2015

MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR KWA TIKETI YA CCM DK. SHEIN,AWATAMBULISHA WAGOMBEA UBUNGE NA UWAKILISHI WA WILAYA YA AMANI UNGUJA


Wasanii wa Kikundi cha Big Star wakitowa burudani kwa wimbo maalum wa Kapeni wakati wa mkutano wa kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein.zilizofanyika katika viwanja vya mpira vya Urafiki mikunguni Unguja
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakiwa katika viwanja vya mkutano wa mkgombea Urais wa Zanzibar kwa kupitia CCM wakishangilia kwa kupeperusha bendera za Chama wakati wa mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya mpira urafiki mikunguni Zanzibar,
Mwanachama wa CCM akishangilia kwa kuonesha picha ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Mhe Borafya Silima akiwahutubia wananchi katika viwanja vya urafiki mikunguni akielezea mafanikio ya CCM yaliopatika kutokana Ilani ya Uchaguzi ya miaka mitano ya Dk Ali Mohamed Shein, wakati wa mkutano wa Mgombea Urais wa Zanzibar uliofanyika katika viwanja hivyo. 
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akizungumza na Balozi Seif Aki Iddi wakiwa katika jukwaa kuu wakati wa mkutano wake wa Kampeni uliofanyika katika Jimbo la Shaurimoyo Wilaya ya Mjini Amani Kichama katika viwanja vya mpira vya urafiki mikunguni. 
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mhe. Haroun Ali Suleima akiwahutubia wananchi na kuzungumzia Ajira wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya CCM Uliofanyika katika Jimbo la Shaurimoyo Zanzibar.
Mbunge wa Jimbo la Kwahani Mhe Dk Hussein Ali Hassan Mwinyi akiwahutubia Wanancxhi katika mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar na kuelezea Ajira kwa Vijana katika Serikali ya Muungano wakati wa mkutano huo uliofanyika katika viwanja vya mipira vya urafiki Zanzibar.
Wanachama wa CCM wakifuatilia mkutano wa Mgombea Urais wa Zanzibar katika uwanja wa mpira wa urafiki mikunguni Zanzibar uliohutubiwa na Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein.

Balozi Amina Salim Ali akiwahutubia Wananchi wakati wa Mkutano wa Kampeni ya mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, uliofanyika katika viwanja vya urafiki na kutowa Salamu za Umoja wa Mataifa kuhusiana na Zanzibar kupiga hatua katika suala la Ajira kwa Vijana. 
Mjumbea wa Kamati Kuu ya CCM Balozi Seif Ali Iddi akiwahutubia wananchi na kuwataka Vijana kupamba maskani zao ili kusherehekea ushindi wa CCM katika uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, na kuelezea jinsi ya mafanikio ya Ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano ya Uongozi wa Dk Shein, ilivyosimamia maendeleo katika sekta mbalimbali za Uchumi wa Zanzibar. na kuwataka kuipigia Kura CCM.chini ya Uongozi wake Dk.Ali Mohamed Shein.
Wanachi wakishangilia wakati Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia na kutangaza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano jinsi itakavyotekeleza mambo mbalimbali katika sekta ya Jamii na kuimarisha maslahi ya Wananchi wa Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, akiwahutubia Wananchi wakati wa mkutano wake wa kampeni ya kugombea Urais wa Zanzibar uliofanyika katika viwanja vya urafiki mikunguni Zanzibar na kuelezea vipaumbele vya Ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano ijayo ya Uongozi wake na kuwaomba kumpigia kura ya NDIO ili kuiongoza Zanzibar kwa mara nyengine tena kutekeleza Ilani hiyo kwa maendeleo ya Uchumi wa Zanzibar . 


Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Amani Zanzibar Mhe Maalim Mussa Hassan wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza AMJADI wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Magomeni Zanzibar Mhe Jamak Kassim Ali wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Mpendae Zanzibar Mhe Salim Turky, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Shaurimoyo Zanzibar Mhe Matari Ali Salum, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi  wa CCM Jimbo la Shaurimoyo, Zanzibar Mhe Hamza Hassan Othman, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Uwakilishi Jimbo la Shaurimoyo Mhe Hamza Hassan akipiga pushap baada ya kutambulishwa na Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, kuonesha afya yake iko safi kwa mazoezi na kutaka kazi ya Uongozi.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa CCM Jimbo la Amani Zanzibar Mhe Maalim Rashid wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa CCM Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Miraji Mussa Kwaza. wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa CCM Jimbo la Magomeni Zanzibar Mhe Rashid Shamsi, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimtambulisha Mgombea Uwakilishi wa CCM Jimbo la Mpendae Zanzibar Mhe Mohammed Salum Dimwa, wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwatambulisha Wagombea Udiwani katika Wilaya ya Amani Kichama wa CCM wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika katika viwanja urafiki mikunguni Zanzibar.


Shekh. akisoma dua baada ya kumalizika kwa mkutanio wa kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar uliofanyika katika viwanja vya moira vya urafiki Jimbo la Shauri moyo Zanzibar.

Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.
Zanzinews.com.
Email. othmanmaulid@gmail.com
Mobile 0777424152 or 0715424152.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages