LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 30, 2015

MAMA SAMIA AWASILI MUSOMA LEO KUENDELEA NA KAMPENI,

 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Musoma, leo asubuhi,  kuendelea na ziara ya kufanya mikutano ya kampeni katika maeneo mbalimbali mkoani Mara. Mama Samia leo anatarajiwa kuhutubia mikutano ya kampeni Sirari,  Mwisenge,  na Sirori Simba.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Damia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwenykiti wa CCM mkoa wa Mara Christopher Sanya baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Musoma, asubuhi hii.


 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan, akisalimia na Mgombea Ubunge jimbo la Musoma Vijijini, Sospeter Muhongo, baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Musoma leo
 Mamam Samia akisalimia baadhi ya viongozi wa CCm, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege mjini Musoma le
 
 Mama Samia akiwa na Ofisa Mwandamizi kutoka Makao makuu ya CCM Juliana Chitinka baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Musoma


Mdau akijaribu kupata picha za Mama Samia
 Msafara wa Mama Samia ukiwa njiani kwenda Sirari, Tarime mkoa wa Mara leo
Msanii wa Bongo Movie, maarufu kwa jina la Bi Mwenda, akihamasisha wananchi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo, Sirari mkoani Mara.
 Wananchi wakimsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Sirari, mkoani Mara
 Wananchi wakiwa na bango kuomba Mamlaka ya Mji Mdogo wa Sirari, Tarime mkoani Mara
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan, akimwelekeza jambo, Mgombea Ubunge jimbo la Tarime Mjini, Michael Kimbaki, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo Sirari mkoani Mara. Kulia ni Mgombea Ubunge jimbo la Tarime Vijijini, Chrisopher Kangoye.
 Wananchi wakimshangilia Mama Samia kwenye mkutano wa Sirari mkaoni Mara
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan, akiwanadi wagombea Ubunge, wa majimbo ya Tarime, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo Sirari mkoani Mara. Kulia ni Chrisopher Kangoye (Tarime Vijijini) na kushoto ni Michael Kimbaki (Tarime Mjini).
 Wananchi wakipiga 'Push Up' kumuunga mkono Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassa, uliofanyika Sirari mkoani Mara.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi y CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwaaga baadhi ya viongozi, baada ya mkutano wa kampeni aliofanya leo, Sirari mkoani Mara. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages