HABARI MPYA

Your Ad Spot

Aug 30, 2015

MAGUFULI KUIPA KIPAUMBELE LUDEWA KWENYE MIUNDO MBINU

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa Fisi kata ya Madaba ambapo alihutubia wakazi wa Madaba kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni na kuahidi kuwa serikali yake itatengeneza Tanzania Mpya .

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli (katikati) akimsikiliza kwa makini  Mhe. Jenista Mhagama (MB) ,mwingine pichani ni Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe.Said Mwambungu wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe.Wiliam Lukuvi akihutubia wakazi wa madaba kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Fisi.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Madaba akihutubia wakazi wa Madaba kwenye mkutano wa kampeni za CCM ambapo aliwaambia wananchi wao akiahidi jambo hutekeleza.
Wananchi wa Madaba wakimsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
Mhe. Jenista Mhagama (MB) akihutubia wakazi wa Jimbo la Madaba kwenye uwanja wa Fisi ambapo alitumia nafasi hiyo kuwaaga rasmi.
Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akisalimiana na Bi.Rosalia Mbelwa mkazi wa Kidodoma ,Madaba mara baada ya kumaliza kuwahutubia wakazi wa Madaba.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimu wakazi wa kata ya Mavanga waliojitokeza barabarani kumsalimia.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimu wakazi wa kata ya Mundindi waliojitokeza barabarani kumsalimia.
 Wakazi wa kata ya Mundindi waliojitokeza barabarani kumsalimia Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwasalimu Watawa wa Kanisa Katoliki waliojitokeza kumsalimu alipokuwa njiani kuelekea Makao Makuu ya Wilaya ya Ludewa  kwenye mkutano wa kampeni za CCM.
Mbunge wa Jimbo la Ludewa Ndugu Deo Filikunjombe akihutubia wakazi wa kijiji cha Itundu, kata ya Mlangali kwenye uwanja wa MTC ambapo aliwaambia wananchi wa kata hiyo kumpigia kura Dk. John Pombe Magufuli kwani ni kiongozi pekee mwenye dhamira ya kuleta maendeleo.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa kijiji cha Itundu kata ya Mlangali ambapo alisema kuwa endapo ataingia madarakani atahakikisha atatoa elimu bure mpaka kidato cha nne,ataboresha huduma za afya pamoja na kuhakikisha haki za msingi za wakulima, walimu na wafanyakazi zitaboreshwa.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli (katikati)akiwanadi mgombea wa ubunge jimbo la ludewa Mhe.Deo Filikunjombe (kushoto) na Mgombea udiwani wa kata ya Mlangali Ndugu Hamisi S. Kayombo
Kikundi cha Ngoma kikitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za CCM mjini Mlangali Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli
Mbunge wa Ludewa Mhe. Deo Filikunjombe akishangilia pamoja na wananchi wengine wakati wa mapokezi ya Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufulikwenye kata ya Mawengi.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na Mbunge wa Ludewa Mhe. Deo Filikunjombe kwenye uwanja wa mikutano Ludewa.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Ludewa kwenye mkutano wa kampeni za CCM ambapo aliahidi kujenga barabara ya lami kutoka Njombe  mpaka Ludewa kwani Ludewa kutakuwa moja ya kitovu cha Uchumi kutokana kuwepo kwa Chuma.
Wananchi wa Ludewa wakimsikiliza Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Ludewa mara baada ya kumkabidhi ilani ya uchaguzi ya CCM Mbunge wa Ludewa Mhe. Deo Filikunjombe kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye viwanja vya michezo Ludewa.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwa amembeba mtoto Shadrack haule mara baada ya kumaliza kuhutubia wakazi wa Ludewa mjini.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages