LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 7, 2015

SAFARI YA KINANA KUTOKA KYAMKWIKWI KWENDA KISIWA CHA BUMBILE, WILAYANI MULEBA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akilakiwa na Mbunge wa Muleba Kusini, Anna Tibaijuka, baada ya kuwasili  Kijiji cha Kyamkwikwi, wilayani Muleba mkoani Kagera leo, kabla ya kupanda boti kwenda Kisiwa cha Bumbile wilayani Muleba.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akibadilishana mawazo na Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka, baada ya kuwasili katika kijiji cha Kyamkwikwi, wilayani Muleba
Mbune wa Muleba Kaskazini,  Charles Mwijage  (kulia) akiselebuka ngoma ya asili na mwenzake wakati wa kumpokea Kinana Kijiji cha Kyamkwikwi

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua ujenzi wa gati katika ziwa Victoria, katika eneo la Kyamkwikwi wilayani Muleba mkoani Kagera
Kinana akipatiwa maelezo kuhusu ujenzi huo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwa na Profesa Anna Tibaijuka katika boti wakati wakijiandaa kusafiri kwenda kisiwacha Bumbile.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiielekeza boti eneo la kutia nanga ili Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wasafiri nayo kwenda Kisiwa cha  Bumbile
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipanda boti kutoka kijiji cha Kywamkwikwi kwenda Kisiwa cha Bubile
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipanda boti hiyo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Nape (kulia) wakiwa na Profesa Anna Tibaijuka wakati safari ilipoanza kwenda Kisiwa cha Bubile.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages