LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 6, 2015

MKUTANO WA KINANA WAFANA MANISPAA YA BUKOBA MJINI

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia wananchi waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza  kwenye uwanja wa Uhuru Platform mjini Bukoba .
Katibu Mkuu wa CCM amefanya ziara katika Jimbo la Bukoba mjini ambapo alitembelea miradi na vikundivya wajasiriamali mbali mbali pamoja na kuhudhuria kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Bukoba mjini.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Bukoba mjini kwenye uwanja wa Uhuru Platform ikiwa sehemu ya muendelezo wa ziara zake za kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi pamoja na kujenga na kuimarisha chama.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu Mkuu wa CCM akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa Manispaa ya Bukoba mjini kwenye uwanja wa Uhuru Platform.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Manispaa ya Bukoba mjini ambapo alikemea baadhi ya watu kutumia Siasa kama njia ya kujinufaisha kinyume na taratibu.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa Manispaa ya Bukoba mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru Platform.

 Mbunge wa Jimbo la Bukoba mjini Balozi Hamisi Kagasheki akiwasalimu wananchi wa jimbo lake kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru Platform.
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Ndugu John Mongella akiwasalimu wananchi wa Bukoba mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa CCM ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alihutubia.
 Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Bw Jackson Musome akiwasalimu wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru Platform.

Msafara wa Pikipiki (bodaboda )kuelekea kwenye uwanja wa mkutano Uhuru Platform ,Bukoba mjini.

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages