LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 13, 2015

KINANA AINGIA WILAYA YA NGARA LEO, AKAGUA MIRADI YAMAENDELEO NA KUTOA CHANJO KWA WATOTO

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpa matone ya chanjo mtoto Benita Cosmas, wakati alipozindua utoaji matone ya chanjo kwa watoto chini ya miezi sita, katika Kituo cha Afya cha Kashinga, kata ya Nyakisasa, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CM na uhai wa Chama katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera, leo. Mama wa mtoto huyo ni Editha Rubambura.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpa kidonge cha chanjo mtotoFrank Laurent, wakati alipozindua utoaji vidonge vya chanjo kwa watoto chini ya mmwaka mmoja, katika Kituo cha Afya cha Kashinga, kata ya Nyakisasa, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CM na uhai wa Chama katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera, leo. Mama wa mtoto huyo ni Janeth Leopard.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akipanda mti wa kumbukumbu, katika Kituo cha Afya cha Kashinga, kata ya Nyakisasa, alipokagua ujenzi wa kituo hicho cha afya akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CM na uhai wa Chama katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera, leo.
Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongela akizungumza na waananchi,  baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana  alipokagua ujenzi wa kituo cha afya cha Kashinga, katika kata ya Nyakisasa, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CM na uhai wa Chama katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera, leo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara aliofanya leo Ngara mjini, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na uhai wa Chama, katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana aliofanyika leo mjini Ngara mkoani Kagera
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipatiwa maelezo kuhusu mradi wa maji katika mji wa Ngara akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM na uhai wa Chama katika mkoa wa Kagera, leo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akijadili jambo na Mkuu wa mkoa wa Kagera, alipokuwa akikagua ujenzi wa mradi wa Umeme Vijijini (REA) katika mji wa Ngara mkoani Kagera leo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizindua chama cha Maendeleo ya Kina mama katika wilaya ya Ngara, kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara mjini Ngara mkoani Kagera leo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikata keki kuzindua akizindua Chama cha Maendeleo ya Kina mama wa Wilayani Ngara mkoani Kagera kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Ngara leo
Wananchi wakishangilia CCM wakati wa mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana aliofanyika leo baada ya mapokezi ya kuingia wilaya ya Ngara akitokea Kyerwa, uliofanyika katika mji mdogo wa Benacc wilayani Ngara
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Benacco baada ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwasili katika wilaya ya Ngara ukitokea Kyerwa kuendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na Uhai wa Chama mkoani Kagera leo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akihutubia mkutanao wa hadhara katika mji mdogo wa Benacco, baada ya kuwasii wilayani Ngara, leo kuendelea na ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na uhai wa Chama mkoani Kagera
Mmmoja wa wakazi wa mji mdogo wa Benacco, kuwa aliwahi kuwa kada wa Chadema akajitoa kutokana na chama hicho kuendekeza amaandamano, akieleza kero walizo nazo wananchi wa mji huo, katika mkutano wa hadhara wa Kinana uliofanyika katika mji huo leo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano wa hadhara aliofanya katika Kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera leo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisaidia kumpatia bati fundi aliyekuwa akipaua, wakati alipotembelea jenzi wa Ofisi ya CCM tawi la Mujebwe, wilayani Ngara mkoani kagera leo
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimwisha ndoo ya maji Francisca Katana, baada ya kuzindua mradi wa maji wa Kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani kagera
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika leo katika Kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera leo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara wa Kinana uliofayika katika kijiji cha Rulenge, wilayani Ngara mkoani Kagera leo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara wa Kinana uliofayika katika kijiji cha Rulenge, wilayani Ngara mkoani Kagera leo
Wananchi wakishangilia katika mkutano wa hadhara wa Kinana uliofanyika katika Kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera
Mmoja wa wazee wa Kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera akiomuonyesha vielelezo kuhusu kero za mashamba zinazowakabili wananchi wa kijiji hicho, leo
Burudai zikiendelea baada ya mkutano mkubwa wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM uliofanyika leo katika kijiji cha Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera leo. picha zote na Bashir Nkoromo

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages